Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kuhusu kuruhusu Taasisi binafsi katika Upimaji Ardhi. Kutokana na uhaba wa fedha katika Wizara kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya Wizara hususan upimaji wa ardhi, naiomba Serikali iruhusu Taasisi binafsi katika kufanya shughuli za upimaji ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa watu binafsi wanatoa huduma kwa wananchi wengi lakini changamoto kubwa ni VAT ambayo wanatozwa na hii hupelekea gharama za upimaji kuwa kubwa, naiomba Serikali iondoe VAT kwenye kampuni hizo za upimaji kusudi gharama za upimaji wa ardhi kwa wananchi zipungue.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa gharama za upangaji wa ardhi ni kubwa na wakati huo huo mtu analipia jengo; na kwa kuwa wananchi wanalipia kodi mara tatu, yaani kiwanja, nyumba na vifaa, naiomba Serikali ibakize kodi mbili tu. Yaani kodi ya kiwanja na kodi ya vifaa vya nyumba ambavyo vinakuwa vimelipiwa na mtu akishajenga jengo. Basi alipie jengo tu na siyo kulipia tena kiwanja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Kanisa la K.K.K.T Njombe Mjini limemilikishwa eneo kubwa hekta 120, katika Kijiji cha Magode na limeachwa bila kuendelezwa na kusababisha mivutano kati ya Kanisa na wananchi wa Magoda; naiomba Serikali ichukue eneo hilo na kuwagawia wananchi wanaohangaika na wamechukuliwa maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.