Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kutoa pongezi za dhati kwa Waziri na Manaibu Mawaziri wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya. Hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia eneo la huduma za afya, Wilaya ya Wanging’ombe imepata fedha za kukarabati Kituo cha Afya cha Wanging’ombe milioni 300 na Kituo cha Afya cha Palangawanu milioni 100. Naomba Serikali itoe fedha milioni 300 ili kukamilisha kazi ambayo kwa sehemu kubwa imefanywa na nguvu za wananchi. Jengo la kituo cha afya na maabara vimeezekwa, jengo la mtumishi kuta zimekamilika, jengo la upasuaji limefikia usawa wa jamvi, jengo la wodi ya wazazi limefikia usawa wa jamvi na jengo la mortuary limefikia usawa wa kuezeka. Ni matumaini yangu Serikali haitaacha kazi hii kubwa bila kukamilisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya hii ina tatizo kubwa sana la huduma za afya. Viko vituo viwili tu vya afya vinavyofanya kazi, hatuna hospitali ya Wilaya ya Serikali. Kwa hiyo tukipata msaada wa kukamilisha Kituo cha Palagawanu kitapunguza tatizo hili. Wilaya inayo maboresho ya zahanati na vituo vya afya ambavyo tumeahidiwa fedha za miradi viporo ili kukamilisha Zahanati za Katenge, Ng’anda, Ivigo, Mtapa, Kanomelenge na Kituo cha Afya cha Igagala hakijaletewa fedha za kukamilisha zaidi ya miaka sita. Naomba pia Serikali itoe fedha za kujenga hospitali ya wilaya ambayo kwa miaka minne tumekuwa tumepangiwa fedha lakini fedha haziletwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la elimu, naomba Serikali isaidie kuboresha Shule ya Sekondari ya Makoga na Wanike ili zisajiliwe kuanza kwa kidato cha V na VI.Wilaya hii imeweza kujenga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kutumia mkandarasi, lakini nyumba mbili zilizokabidhiwa TBA toka mwaka 2012 mpaka leo ziko hatua ya msingi na kazi imesimama. Nyumba hizo ni kwa ajili ya makazi ya Mkuu wa Wilaya na Afisa Tawala. Mkuu wa Wilaya anaishi nyumba ya kupanga toka Wilaya hii ilipoanzishwa 2011. Naomba Serikali itoe kibali kwa kutumia utaratibu wa kuajiri wakandarasi ili viongozi hawa waishi kwenye nyumba za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii na kutegemea maombi yangu kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe yatazingatiwa.