Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na kumpongeza Waziri Mheshimiwa Jafo kwa kazi nzuri sana ambayo amekuwa akiifanya. Pia niwapongeze Naibu Mawaziri Mheshimiwa Kakunda na Mheshimiwa Kandege bila kumsahau Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bila malipo, nimpongeze sana kwa sera yake ya elimu bila malipo kwa sababu imesaidia vijana wengi kupata nafasi ya kusoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie changamoto katika shule za msingi katika Mkoa wa Iringa. Ukarabati wa majengo na miundombinu, majengo ya shule za msingi yana hali mbaya sana sababu halmashauri nyingi zinaweka vipaumbele katika ujenzi wa sekondari na maabara kutokana na ufinyu wa bajeti zilizopo katika halmashauri.

Changamoto nyingine katika shule hizi ni malipo ya maji, umeme na walinzi na hii inasababisha hata vyoo kutotumika. Naomba Serikali kama ilivyotoa malipo kwa ajili ya elimu iondoe pia gharama za maji na umeme mashuleni, shule zina bills kubwa sana wanakatiwa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ucheleweshwaji wa fedha katika miradi ya maendeleo katika halmashauri. Serikali iangalie miradi yenye tija katika halmashauri zetu ili iweze kuleta pesa kwa wakati katika halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa machinjio ya kisasa Iringa Manispaa. Mradi huu ni wa muda mrefu sana, tulianza toka 2008 unahitaji sasa 1.4 bilioni. Ni chanzo kizuri sana, mapato katika halmashauri yetu na ukimalizika utaweza kutoa ajira kwa wananchi zaidi ya 200. Ni vyema tukae na miradi michache na tuwe na miradi ya vipaumbele kuliko kuwekeza pesa kidogo katika miradi mingi ambayo inachelewa kukamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA naipongeza Serikali kwa kuamisha huu wakala kwa ajili ya kushughulikia barabara za halmashauri ningeomba Serikali iiwezeshe TARURA kutengewa bajeti ya kutosha ofisi, wataalam na vifaa kama magari kwa sababu pamoja kazi kubwa waliyonayo bado wanapata shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Manispaa yetu ya Iringa kuna mradi wa Daraja la Tagamenda lipo Igumbilo. Daraja hili limechukua muda mrefu sana, kuna majanga huwa kila mwaka yanatokea maafa makubwa, vifo, sababu kuna shule ya sekondari na wananchi ambao wanategemea
kutumia daraja hilo. Sasa tumeambiwa daraja hilo limehamishiwa TARURA, ningependa kupatiwa majibu, tulipohoji katika manispaa yetu tuliambiwa Serikali imeleta fedha ya kutosha kumaliza daraja, hilo je, ni kweli na je, daraja hilo lini litakamilika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali kwa mgao wa shilingi 4.5 bilioni zilizotengwa wa ajili ya hospitali zetu za Mkoa wa Iringa, Hospitali ya Kilolo, Mufindi na Iringa DC. Hospitali yetu Iringa Manispaa haijatengewa pesa yoyote na kuna changamoto kubwa sana ya jengo la vipimo, pia hakuna mashine za x-ray, T-scan, ultrasound, hakuna ward za kulaza wagonjwa wengine kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali ya mkoa. Pia tunamshukuru sana Waziri wetu, Mheshimiwa Jafo alipita na aliona hiyo changamoto. Naomba Serikali ilichukue hilo kwa uzito.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.