Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimwa Mwenyekiti, naomba kuchukua nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha ktupaa nafasi ya kuchangia Wizara hii muhimu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora. Nipende kumpongeza sana Waziri wa Utumishi Kapteni George Huruma Mkuchika kwa kazi kubwa anayoifanya ya kusimamia Utumishi wa Umma. Nakiri kwa kusema nidhamu ya utumishi wa umma imerudi na uwajibikaji umeongezeka kwa kiwango cha juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kaulimbiu ya Awamu ya Tano ni uwekezaji katika viwanda unaochochea ukuaji wa nchi. Ili kuwekeza katika viwanda lazima tuwe na rasilimali watu tuliyoiandaa kikamilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma ndiyo inayoratibu na kusimamia utumishi wa umma nchini. Utumishi wa umma unatakiwa kuwa endelevu, unatunza historia na kumbukumbu za Serikali hali kadhalika utumishi wa umma unatakiwa kutekeleza kazi za Serikali iliyoko madarakani bila kujali inatokana na chama gani cha siasa ili kuondoa uwezekano wa mtumishi kutoa huduma kwa upendeleo au ubaguzi kutokana na itikadi za kisiasa. Kuingiza utumishi wa umma katika itikadi za vyama kutayumbisha utumishi wa umma ambao ndiyo injini ya utendaji wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii tena kumpongeza Waziri na viongozi wote kwa ujumla kwa maamuzi ya kurudisha kazini watumishi wa darasa la saba, walioondolewa kazini. Kwanza hii niseme inapunguza gharama kubwa kwa Serikali kuwalipa watumishi hawa. Sambamba na hilo hawa watajifuta wenyewe kwa kuwa baada ya elimu bure Watanzania wengi watatoka hapo na kufikia angalau kidato cha nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watumishi hawa wametumikia Serikali kwa muda mrefu kwenye fani ya udereva na uhudumu wa ofisi nyingi za Serikali yetu. Nimekuwa mtumishi katika Hifadhi za Taifa Tanzania na watumishi wengi walioko kwenye level ya darasa la saba ndiyo walinzi wakubwa wa rasilimali zetu, maliasili za Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nizungumzie upungufu wa watumishi, Wataalam kwenye Wizara ya Afya. Hili limekuwa na changamoto kubwa kwenye Idara ya Afya na hivyo kupelekea hospitali zetu za rufaa kubeba mzigo mkubwa. Nashauri eneo hili liangaliwe kwa jicho la pekee sana.