Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nipongeze Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa maamuzi yenye busara na haki katika kazi za kuhudumia halmashauri zetu. Pamoja na hayo nilete ombi la kutekelezwa kwa ujenzi wa kilomita tano katika Mji wa Haydom ambapo Rais aliahidi kujengwa kwa kiwango cha lami na Dongobeshi kilomita mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata fedha za kituo cha Afya cha Dongobeshi. Naomba kupewa tena fedha katika Kituo cha Maretadu, Endamilay, Masieda na Maghangw kwani wananchi wanapata tabu ya kutembea mbali kutafuta huduma ya hospitali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA; Jimbo la Mbulu Vijijini lina changamoto kubwa ya barabara na madaraja ambayo hayapitiki. Naomba TARURA Wilayani ipewe kipaumbele cha kupewa bajeti zaidi ili kutatua au kupunguza changamoto hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Watumishi; tuna changamoto ya kutokuwa na Engineer wa Maji; Idara inakaimiwa na Fundi Mchundo. Walimu wa Sayansi hatuna kwa kiwango kikubwa, hivyo tunaomba tupatiwe pia Maafisa Kilimo na Mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kwa umuhimu wa pekee, napenda sasa kuishukuru Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mawaziri wake wamefanya ziara katika wilaya yetu. Nawashukuru sana Mheshimiwa Jafo, Mheshimiwa Joseph Kakunda na Mheshimiwa Joseph Kandege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu; wawe na mpango wa kuwaelekeza Watendaji Wakuu mfano, DC, DED, RC, wajue sheria za Serikali za Mitaa na kuziheshimu hasa PPRA, RRA na D-by D ili wafahamu utaondoa mikanganyiko iliyopo huko maana inaleta taswira mbaya na kuchafua picha nzuri ya Serikali bila sababu kwa wananchi. Tusiposhughulikia tunaweza kupoteza ari na kutoungwa mkono kwa Serikali na chama chetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.