Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuwa miongoni mwa washiriki katika mjadala wa bajeti 2018/2019. Naipongeza Wizara ya TAMISEMI kwa kufanya kazi vizuri chini ya uongozi wa Mheshimiwa Waziri na Manaibu wake pamoja na watendaji wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona juhudi za Serikali katika suala la afya na kuongeza juhudi katika ujenzi wa zahanati. Naiomba Serikali iendelee kutoa mchango wake katika zahanati na maeneo ya visiwani. Naomba nielezee zilizopo Mkoa wa Pwani Wilaya ya Rufiji, Kibiti, Mkuranga na Mafia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamii inayoishi kwenye visiwa inahitaji huduma zote muhimu katika maeneo yao ikiwemo afya na usafiri wa uhakika ambao ni haki yao kwa kuwa maeneo mengine kuna aina mbliambali za usafiri. Naomba Serikali iongeze nguvu au kupeleka usafiri wa boti la wagonjwa kwa wananchi wa Kisiwa cha Koma na Kwale vilivyopo Wilaya ya Mkuranga ili kuokoa na kurahisisha usafiri kwa wagonjwa hususani kwa wajawazito, watoto na wengine wanapougua ukizingatia mama mjamzito anapotoka kujifungua hajui muda gani wala siku. Kusipokuwa na huduma sahihi na za haraka hupelekea kupoteza maisha na hivyo inatokea sana kwenye visiwa vyetu vya Mkoa wa Pwani. Chondechonde naiomba Serikali itupatie huduma hiyo au kupeleka vifaa vyote muhimu vya tiba na wahudumu muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ya TAMISEMI izielekeze Halmashauri zote ziweze kutenga fedha kwa ajili ya taulo za wasichana mashuleni ili kuwawezesha wale wasio na uwezo wa kuzipata na kushindwa kuhudumia masomo pia kuwa na ufaulu usioridhisha kwa watoto wa kike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili linawezekana kwani Halmashauri ya Kisarawe imeanza kutenga fedha hizo kwa mantiki hiyo, Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe na nyingine ambazo zimekuwa zinatenga fedha. Nimelisema hilo kwa kuwa ni tatizo kubwa sana kwa baadhi ya wanafunzi wa kike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kutoa fedha na kukarabati shule Kongwe nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali katika juhudi zake za kusogeza maendeleo jamii na kuziwezesha. Suala la kupunguza riba kwenye mikopo ni jambo jema sana, hivyo basi mchakato wake ukamilike kwa haraka ili ulete unafuu kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA; iwezeshwe ili iweze kufanya kazi zake kwa wepesi. Mkoa wa Pwani unahitaji barabara zake ziwe za kupitika mwaka mzima kwani zitarahisisha maendeleo na pia kuwezesha kusafirisha malighafi na bidhaa zinazotoka kwenye viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.