Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naungana na wachangiaji waliotangulia kuwapongeza Waziri na Naibu Mawaziri kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara hii. Nianze na kuchangia kuhusu Walimu. Walimu wanafanya kazi nzuri na ni walezi wa pili katika familia baada ya wazazi/walezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda mwingi Walimu wanashinda na watoto wanaotoka katika malezi mbalimbali lakini wanapofika shuleni wao huwa ndiyo walezi, Madaktari, Manesi, Mahakimu, Polisi na kadhalika. Kazi zote hizi Walimu wanakuwa kama ndiyo mbadala wa watajwa hapo juu kutokana na majukumu wanayoyafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu ndiyo chimbuko la wafanyakazi wa fani zote katika nchi hii. Kama Mwalimu angeacha kumpatia mwanafunzi msaada wa kumudu kusoma vizuri darasani akafaulu vizuri na hatimaye kufika hadi chuo kikuu na kuweza kupata kazi nzuri ya kumwendeshea maisha yake au hata kuweza kujiajiri mwenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwalimu huyu yuko katika mazingira magumu sana lakini bado wanaendelea na mikakati ya kufundisha ili kujenga Taifa la wasomi. Naiomba Serikali angalau iwarudishie Walimu ile posho waliyokuwa wakipewa miaka ya 80 yaani teaching allowance. Hii teaching allowance, ilikuwa ni asilimia 25 ya mshahara wa Mwalimu. Hii ingewasaidia Walimu katika kupunguza makali ya maisha na kumudu kufanya vizuri kazi yao ya kuwafundisha watoto.