Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kuwarudisha kazini wale wote ambao waliachishwa kazi kwa sababu ya kuwa na elimu ya darasa la saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali iangalie kwa jicho la huruma hospitali ya Rufaa ya Mtwara. Katika hospitali hii kuna upungufu mkubwa wa Madaktari pamoja na Wauguzi. Hospitali hii inahudumia wagonjwa wengi sana kutoka maeneo mengi sana ya Mkoa wa Mtwara. Katika hospitali pia kuna upungufu mkubwa wa dawa.

Naomba hospitali hii iongezewe bajeti ili wananchi wa Mkoa huu wa Mtwara waweze kupata dawa na huduma za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za vijana/ akinamama. Kwa mujibu wa sheria, kila halmashauri ina majukumu ya kutenga asilimia 10 kwa ajili ya vijana asilimia tano na akina mama asilimia tano. Hata hivyo, kwa kuwa vyanzo vya mapato ya kodi za majengo (property tax) na ushuru wa mabango vimechukuliwa na TRA, Halmashauri haziwezi kutoa fedha za mikopo kwa akinamama na vijana. Hii inasababisha vijana na akinamama kuchukua mikopo BRAC, FINCA na kadhalika. Taasisi hizi zina riba kubwa na akinamama wanachukuliwa vyombo vyao vitanda, makochi, TV, radio na kadhalika pale wanaposhindwa kulipa riba hizo.