Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ufafanuzi na msimamo wa Serikali katika mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Tanga, Wilaya ya Muheza ina upungufu wa Walimu wa shule ya msingi 487, kwani waliopo ni 846 na mahitaji ni 1,333. Je, Wizara ina mkakati gani kuipatia Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Walimu hao 487 ili kujenga msingi imara wa kielimu kwa watoto wetu wa shule za msingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa nyumba za Walimu ni mkubwa sana Wilayani Muheza, Serikali imejipangaje kuanzisha mpango mkakati wa haraka kusaidia kutatua changamoto ya makazi ya watumishi. Makazi ya askari polisi ni duni, chakavu na hayatoshi. Je, Serikali imejipangaje kutatua changamoto hiyo kubwa inayopunguza morali ya askari wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, afya; upungufu wa watumishi katika hospitali teule Wilayani Muheza, Serikali tunaomba mtufikirie. Katika hospitali ya Muheza (Teule) dawa ya nyoka ni 250,000 x3 na dawa ya mtu aliyeng’atwa na mbwa ni 50,000x3. Mheshimiwa Waziri, kung’atwa na mbwa na kung’atwa na nyoka ni ajali ambazo asilimia kubwa ni wananchi waishio vijijini (mashambani). Je, Serikali haioni ni wakati muafaka dawa hizi kuziingiza kwenye kundi la dawa muhimu ili wananchi wazipate bure. Serikali iliahidi katika mwaka wa fedha 2016/2017 imetenga milioni 20 kwa ajili ya ambulance na mpaka sasa gari huko la wagonjwa halijafika Muheza katika Hospitali Teule. Je, ni lini tutapata gari la wagonjwa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utumishi; katika Wilaya ya Muheza wapo watumishi waliosimamishwa kazi na Serikali kwa sababu mbalimbali. Wapo wengi wa darasa la saba walinzi, madereva na watendaji wengine. Je, Serikali imejipangaje kuwalipa stahiki zao kwa wakati na kuwarudisha kazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, posho kwa Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji kwani wanafanya kazi kubwa ya kuwahudumia wananchi lakini hawapati chochote. Je, Serikali imejipangaje kuwapa posho ili nao wapate utulivu wa kufanya kazi zao.