Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa hotuba nzuri. Vile vile pongezi kwa Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na Naibu Makatibu Wakuu na watumishi wote wa Wizara kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ni juu ya utekelezaji wa ahadi za Mheshimiwa Rais katika Jimbo la Busanda. Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga barabara ya lami yenye urefu wa kilometa tano katika mamlaka ya Mji Mdogo Katoro na kilometa tano Buseresere wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015. Mpaka sasa ni miaka mitatu hakuna kinachoendelea. Ningependa kujua ni lini ujenzi wa barabara hizi utaanza rasmi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ujenzi wa barabara katika Jimbo la Busanda kuna kero kubwa sana ya upatikanaji wa maji safi na salama. Kwa kuwa mamlaka ya Mji Mdogo Katoro kuna idadi kubwa sana ya watu na suala la maji ni kero kubwa ambapo tumezungukwa na Ziwa Victoria. Naomba Serikali iwe na mkakati maalum wa kuvuta maji kutoka Ziwa Victoria ili kupata suluhu juu ya changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama. Kwa maneno machache naomba kuwasilisha ili Serikali iweze kutafutia ufumbuzi changamoto hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Ahsante.