Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutopandisha watumishi madaraja licha ya kuwa na sifa stahili mfano kuna watumishi 8,369 katika mamlaka 18 hawajapandishwa kwa mujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali mpaka 30 Juni, 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa watumishi katika Halmashauri 161 ambao ni takribani 155,013 sawa na 32% ya huhitaji ambao ni takribani 500,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutopelekwa 10% ya own source (mapato ya ndani) katika Halmashauri 143. Ushauri wangu kuwepo na akaunti maalum na hii pesa iwekwe huko kwanza hata kabla ya matumizi ya kawaida mengine kupewa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakusudia kuja na hoja binafsi kuishawishi Serikali kuleta Muswada wa kuzibana Halmashauri ili pesa hii ipelekwe kwa kundi hili maalum katika jamii yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri kuendelea kupanga bajeti zisizo halisi, ndio maana Halmashauri nyingi zimelazimika kuongeza bajeti zake. Mfano Ilala 10%, Mlele 51% na ya kusikitisha ni Newala 81%, kweli bajeti ina-burst kwa 81%.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutopelekwa fedha za maendeleo, hata zile zilipelekwa zimechelewa. Hii inarudisha nyuma juhudi za wananchi kujiletea maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, halmashauri tatu kuendelea kufanya vibaya. Je, watumishi waliopo hawaendelezwi kielimu au ni wezi?