Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la masomo ya sayansi katika sekondari. Mahitaji Walimu 35,136, waliopo 19,459 upungufu 15,677; je, Tanzania ya viwanda itafanikiwa kwa hali hii? Serikali imefanya sensa ya Walimu wa sayansi wanaoacha kazi katika shule za sekondari na kujua sababu zilizopelekea kuacha kwao na kujua namna ya kuzitatua kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Mfuko wa Wanawake na Vijana. Kwa nini katika Halmashauri hakuna akaunti maalum kwa ajili ya fedha hizi, mwisho wake lini Halmashauri kuchangia Mfuko huu kwa sababu huu Mfuko fedha zake zinazunguka. Ni matarajio yangu kwamba baada ya muda Mfuko huu uweze kujiendesha na fedha zinazotolewa na Halmashauri ziweze kufanya au kutoa huduma nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila halmashauri ina chanzo kimoja cha uhakika ambacho ni ardhi, lakini Serikali Kuu imekuwa ikichukua fedha hizo na kushindwa kurudisha 30% inayotakiwa kwenye halmashauri. Je, hapa Serikali Kuu inatenda haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni ya Kamati yanasema halmashauri nyingi zimeshindwa kukusanya mapato hata chini ya 25% na kushauri Halmashauri hizo zitafute vyanzo vingine vya mapato. Je, vyanzo hivyo vinatoka wapi ikiwa kila chanzo halmashauri zinazobuni Serikali Kuu inachukua? Je, vyanzo hivyo vipya vya mapato ya Halmashauri vinavyotakiwa kubuniwa ni kama vipi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mradi wa utekelezaji wa Manispaa ya Mtwara Mikindani. Taa zilizofungwa katika barabara ya Zambia haziwaki, naomba ufafanuzi wa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha ujenzi wa stendi ya kisasa katika eneo la Mkanaledi, Manispaa ya Mtwara Mikindani. Stendi iliyopo sasa ni ndogo haikidhi mahitaji, naomba ufafanuzi kuhusu hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kuwasilisha.