Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja ya Ofisiya Rais, Utumish na Utawala Bora kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie katika utawala bora; kumekuwa na tatizo la Wakuu wa Wilaya kuwanyanyasa Madiwani na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa. Mfano; Mkuu wa Wilaya ya Njombe amekuwa anaingilia vikao vya Madiwani na kutoa amri zisizo na tija kinyume na kanuni. Naomba wakuu hao wapewe maelekezo wasivuruge Baraza la Madiwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Utumishi; watumishi kutopewa maslahi stahiki; kuna watumishi ambao wamepandishwa madaraja lakini mishahara yao imebaki ile ile, mfano Wlimu. Naomba Serikali iwapandishe madaraja, lakini pia wapandishwe mishahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie Ofisi ya Rais, TAMISEMI kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Waziri wa TAMISEMI kwa moyo wake wa kujituma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Elimu Bure/Bila Malipo; kumekuwa na mkanganyiko mkubwa katika utekelezaji wa matamko ya viongozi wa juu wa Serikali. Matamko hayo yamekuwa yakitolewa bila kufanyiwa utafiti; matamko hayo yamekuwa yakiathiri wananchi. Mfano, Rais alipotamka kuwa wanafunzi wasitozwe kitu chochote, wazazi walikwenda shuleni na kudai fedha zao za michango na vyakula ili kurudishiwa. Hivyo, naiomba Serikali ihakikishe inapotamka ifanye utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wa sekondari kwenda kufundisha shule za msingi; kumekuwa na changamoto kubwa kwa kuhamisha Walimu wa sekondari kwenda kufundisha shule za msingi. Kwanza walimu hawa waliandaliwa kwa ajili ya kufundisha wanafunzi wakubwa na siyo watoto wadogo. Hivyo, inakuwa vigumu sana watoto hawa wadogo kuwaelewa Walimu hawa wa sekondari na hii itasababisha watoto kufeli. Naiomba Serikali iajiri Walimu wanaolingana na ufundishwaji wa shule za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyanzo vya mapato vya halmashauri kuchukuliwa na Serikali Kuu; Serikali Kuu imechukua vyanzo muhimu vya halmashauri. Kwa mfano, ardhi ndiyo rasilimali pekee ambayo kila halmashauri inamiliki; ardhi ndicho chanzo cha mapato cha uhakika kwa kila halmashauri ya nchi hii. Halmashauri zinatakiwa kuchukua asilimia 30 ya kodi ya ardhi, lakini Serikali imechukua kodi hiyo na fedha hizo hazirudishwi na zikirudishwa zinarudi kwa kuchelewa. Naiomba Serikali kurudisha baadhi ya vyanzo vya mapato katika halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo; wananchi wamehamasika wamelima mazao ya mahindi, matunda, nazi na mazao mengine. Wamejitoa kununua mbolea, dawa za wadudu na kutunza mazao yao kwa gharama kubwa na hatimaye wamevuna kwa wingi lakini hakuna soko. Kwa mfano, wananchi wa Ludewa katika Mkoa wa Njombe wanategemea sana zao la mahindi ambalo limekuwa likichukuliwa na watu NFRA, lakini mwaka huu hawajachukua mahindi hayo. Naiomba Serikali itafute soko kwa ajili ya wananchi wetu kwa kufungua mipaka ili mazao hayo yauzwe nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maji; miradi ya maji katika halmashauri nyingi inasuasua; mfano, katika Halmashauri ya Mji wa Njombe kuna Miradi ya Maji ya Lugenge na Hagafilo, inasuasua. Naiomba Serikali ifuatilie miradi hiyo na kubaini tatizo linaloikwamisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bili za maji zimekuwa ni tatizo kubwa; zinaletwa bili kubwa wakati maji yanayotumika ni kidogo. Pia kumekuwa na uchakavu wa mabomba, mfano maeneo ya Kisasa mabomba yanapasuka ovyo. Naiomba Serikali ifuatilie suala hili la uchakavu wa miundombinu ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.