Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, uhaba wa Walimu wa sayansi, Sekondari Kakonko. Nchi nzima ina uhaba wa Walimu wa sayansi wa sekondari zaidi ya 15,000. Kwa mantiki hiyo sera ya uchumi wa viwanda ni ndoto nchini maana wataalam watakuwa hawapo kutokana na ukosefu wa sayansi. Kakonko kuna upungufu. Ushauri ni Serikali iajiri Walimu wa sayansi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu ya mashuleni; kuna uhaba mkubwa mashuleni wa miundombinu, kama ifuatavyo: Nyumba za Walimu, vyumba vya madarasa, vyoo vya wanafunzi na Walimu, madawati, maabara, viwanja vya michezo na vifaa vya michezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madai ya Walimu; Walimu wana madai mengi yasiyolipika. Hali hii inakatisha tamaa Walimu na kushusha morali ya kazi. Ushauri ni Serikali ilipe madeni yote ya Walimu ili waongeze tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa Hospitali ya Wilaya Kakonko; Wilaya ya Kakonko haina hospitali ya wilaya na sasa Kituo cha Afya cha Kakonko kimeelemewa sana. Kituo hicho kinapata dawa kwa hadhi ya kituo cha afya wakati kinahudumia wagonjwa kwa ngazi ya wilaya, hivyo kuishiwa dawa mapema. Pia, dawa muhimu zinaletwa kwa level ya kituo cha afya. Nashauri kwamba, Serikali ijenge Hospitali ya Wilaya Kakonko mwaka 2018/2019. Pia Kituo cha Afya Gwanumpu kifanyiwe ukarabati, kwani kilitengewa fedha 2017/2018 lakini fedha hazikutoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Watumishi wa Afya. Kuna upungufu mkubwa sana wa watumishi wa sekta ya afya, jambo linalotishia afya za Watanzania sambamba na vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga. Nashauri Serikali iajiri watumishi wa sekta ya afya. Ukosefu wa watumishi wa sekta ya afya kwenye vituo vilivyojengwa na Bloombergy vipatavyo vitano kwa ajili ya baba, mama na mtoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Miradi ya Maji ya World Bank iliyokwama. Kuna miradi mitano ya maji ambayo imekamilika, lakini haitoi maji. Miradi hii ilishalipiwa fedha zote mpaka za retention, lakini hakuna maji. Miradi hiyo ya World Bank ni kama ifuatavyo:-

(i) Mradi wa Maji Nyagwijima, Kata ya Mugurunza;
(ii) Mradi wa Maji Kiduduye, Kata ya Nugunza;
(iii) Mradi wa Maji Katanga, Kata ya Katanga;
(iv) Mradi wa Maji Muhange, Kata ya Muhange; na
(v) Mradi wa Maji Kiga, Kata ya Ruyeye una nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi hii ichunguzwe haraka. Nashauri wasimamizi na wakandarasi waliohujumu miradi hii wachukuliwe hatua za kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nichangie Ofisi ya Rais, Utumishi kama ifuatavyo:

Upungufu mkubwa wa watumishi; uhaba wa Walimu shule za msingi about 95,000, uhaba mkubwa wa Walimu wa Sayansi (sekondari) zaidi ya 15,000, uhaba mkubwa wa watumishi wa Sekta ya Afya. Nashauri Serikali itoe ajira Wizara ya Elimu na Afya ili kukidhi mahitaji ya watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Utawala bora; utawala wa sheria (rule of law); kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi na Katiba ya nchi kwa ujumla. Mfano, kuzuia mikutano ya hadhara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie kuhusiana na uhuru wa mawazo. Wanaoikosoa Serikali au kuishauri wanapata misukosuko na wengine kupotezwa. Mfano Azori, Ben Saanane na kadhalika; watumishi wa kiroho kupata misukosuko baada ya kuhoji kuwepo kwa Katiba mpya au Serikali kukosolewa kwa maslahi ya Taifa. Mfano, Maaskofu Niwemugizi na Kakobe kufikia kuhojiwa uraia wao kwa sababu hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni ukiukwaji wa haki za binadamu tena za kikatiba. Magazeti yanafungwa na Waandishi wa Habari kukosa uhuru wa kuandika taarifa zao; TV kutozwa faini kwa sababu ya kutoa taarifa zisizoipendeza Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukosekana haki ya kuishi; tumeshuhudia wananchi wakipoteza maisha na maiti zao kuonekana zinaelea baharini na Serikali iko kimya; mauaji ya mwanafunzi Akwiline Akwilini; mauaji ya Daniel, kiongozi wa CHADEMA, Kata ya Hananasifu na maiti yake kutupwa Fukwe za Coco Beach.