Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwenye mapitio ya utekelezaji wa mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ukurasa wa saba, tunaona ufafanuzi wa fedha iliyoidhinishwa kwa mwaka 2017/2018 ni trilioni 6.57 kwa ajili ya mishahara, matumizi mengineyo na miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hiyo tunaona mishahara ni trilioni 4.27 ila jumla ya fedha zilizopokelewa kufikia Februari, 2018 ni trilioni 3.33 sawa na asilimia 50.68 ya bajeti yote iliyoombwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, utoaji wa fedha iliyobakia utatolewa ndani ya kipindi hiki kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha, sababu tukiangalia muda uliotumika kutoa fedha iliyotolewa ni mwingi na fedha iliyotolewa inaonesha haitoweza kutosheleza hata bajeti ya mishahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ajira ni la muhimu katika Taifa, hasa tunaposema tunahitaji nchi ya viwanda, tutaendaje kupata product ya wataalam wa kuendeleza hivi viwanda siku za mbele endapo Walimu mashuleni hakuna, Walimu wa sayansi hakuna wa kutosha. Je,
tutapataje product yetu wenyewe ya kuendeleza viwanda vyetu endapo hatuajiri Walimu wa kutosha kutoka ngazi ya msingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ifanye mikakati ya makusudi ya kuajiri walimu kuanzia ngazi ya msingi na pia kuwatengenezea mazingira mazuri Walimu sehemu wanazopangwa kwenda kufundisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia suala la utawala bora nchi yetu inatakiwa isimamie kwenye misingi ifuatayo:-

Kuzingatia utawala wa sheria, kuzingatia busara na kuzingatia heshima. Ila kwa mwenendo wa sasa unaoendelea wa kila mtu anasema anachokifikiria yeye italeta shida. Mfano tumeshuhudia Wakuu wa Wilaya wakiwaweka Wabunge ndani na kuwafukuzisha watu kazi bila kufuata utaratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Waziri mwenye dhamana, Wakuu wa Wilaya, Mikoa na Wakurugenzi wanaochukua hatua bila kujali taratibu wachukuliwe hatua za kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nizungumzie Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora kama ifuatavyo:-

Suala la ajira ni la muhimu katika Taifa hasa tunaposema tunahitaji nchi ya viwanda tutaendeleaje kupata product ya wataalam wa kuendeleza hivi viwanda siku za mbele endapo Walimu mashuleni hakuna? Walimu wa sayansi hakuna wa kutosha, je, tutapataje product yetu wenyewe ya kuendeleza viwanda vyetu endapo hatuajiri Walimu wa kutosha kutokea ngazi ya msingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ifanye mikakati ya makusudi ya kuajiri Walimu kuanzia ngazi ya msingi na pia kuwatengenezea mazingira mazuri Walimu sehemu wanazopangiwa kwenda kufundisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia suala la utawala bora nchi yetu inatakiwa isimamie kwenye misingi ifuatayo:-

Kuzingatia utawala wa sheria; kuzingatia busara na kuzingatia heshima. Kwa mwenendo wa sasa unaoendelea wa kila mtu anasema anachokifikiria yeye italeta shida. Mfano tumeshuhudia Wakuu wa Wilaya wakiwaweka Wabunge ndani na kufukuzisha watu kazi bila kufuata utaratibu. Nashauri Waziri mwenye dhamana, Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wanaochukua hatua bila kujali taratibu za ajira wachukuliwe hatua za kisheria.