Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Nkansi ina eneo kubwa sana la Ziwa Tanganyika na kuna aina nyingi za samaki na hata dagaa, lakini wavuvi wengi karibu wote hali zao ni mbaya sana hawana zana bora za uvuvi kabisa. Wavuvi wengi au karibu wote ni raia kutoka DRC-Congo ndiyo wanaofaidika na maliasili ya Ziwa Tanganyika, maana Vijiji karibu vyote vya mwambao mwa Ziwa Tanganyika upande wa Tanzania ni wavuvi kutoka DRC-Congo.
Mheshimiwa Naibu Spika, je, kuna halali gani Wakongo kuwa upande wa Tanzania bila hata uhalali wa kukata leseni zinazostahili wageni toka DRC-Congo? Naomba Wizara yako ichukue hatua kwa wageni wote wanaokwenda kinyume, pia wale waliopewa majukumu huko. Nadhani wanafanya kutotekeleza sheria kwa ajili ya kupewa chochote na hao wavuvi wageni. Hata uvuvi haramu kwa kutumia nyavu zilizopigwa marufuku mwambao mwa Ziwa Tanganyika wamezagaa Tanganyika karibu kila kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Nkasi kuna mapori shamba kama vile waliohodhi hawayatumii na walipata kwa kuwarubuni Wenyeviti wa Vijiji, wakati hakuna sheria wao kutoa ardhi zaidi ya hekari 50. Unakuta kuna mashamba pori ya hekari 100 na kuendelea. Mfano; shamba la Kowi, Kalumwalwedo,shamba la Msomali Tatumbila, shamba la Mastar Mashete, mashamba yote hayo yalipatikana kwa vijiji kukiuka sheria ya uwezo wao wa hekari 50 tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna baadhi ya wafugaji walipewa block katika shamba, yaani Ranch ya Kalambo lakini hawajapeleka mifugo na wanakodisha hizo block tu, Wizara ikalitazame upya na kuwapatia wafugaji wenye ng‟ombe.