Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hotuba ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI kama ifuatavyo:-

Kwanza ni mgao wa Wilaya. Wilaya ya Tunduru ina eneo kubwa sana la utawala ambalo linalingana na eneo la Mkoa wa Mtwara wenye Wilaya Sita. Tunaomba Serikali ifikirie suala la kugawa Wilaya ya Tunduru ili kurahisisha shughuli za kuhudumia wananchi kwa kuleta huduma karibu na wananchi. Kila eneo la Jimbo liwe Wilaya kamili inayojitegemea kutokana na wingi wa watu na umbali kutoka Makao Makuu ya Wilaya ilipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tatizo la watumishi wa Halmashauri. Tuna upungufu mkubwa wa watumishi wa Halmashauri katika sekta zote za afya, elimu na kada zingine za kilimo. Tuna upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi zaidi ya 1,000 na Walimu wa Sayansi wa Shule za Sekondari zaidi ya 100 na kuna upungufu wa watumishi wa afya zaidi ya 700, tuna watumishi asilimia 26 tu katika Sekta ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watumishi wa Halmashauri wamekuwa na muda mrefu katika Halmashauri ya Tunduru na wanasababisha kudumaa kwa kazi za Halmashauri na wanafanya kazi kwa mazoea. Hivyo, tunaomba watumishi waliokaa muda mrefu wahamishwe, wapelekwe Halmashauri zingine ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vituo vya afya. Halmashauri ya Tunduru ina Kata 35 ina vituo vya afya vitano tu. Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kituo cha afya Nalasi lakini mpaka leo kuna msingi tu. Wananchi walifyatua tofali za udongo lakini tangu 2014 mpaka leo hamna kinachoendelea. Halmashauri inatenga fedha kila mwaka lakini hazipatikani kabisa, hivyo naomba Kituo hicho cha Afya Nalasi ambacho kitahudumia Kata mbili za Nalasi Magharibi na Nalasi Mashariki zenye wakazi zaidi ya 30,000 kijengwe na Serikali ili kuheshimu ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na kituo hicho naomba Serikali isaidie Halmashauri kujenga vituo vya afya angalau vinne zaidi kupunguza adha ya huduma kwa akinamama na watoto. Kata hizo ni Malumba, Lukumbule, Ligoma, Misechela na Tuwemacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la nne ni maji. Kuna tatizo kubwa la maji katika maeneo mengi ya Jimbo la Tunduru Kusini, kutokana na mabadiliko ya tabianchi mito mingi imekauka kabisa hasa katika Vijiji vya Mchoteka, Likweso, Mnemasi, Molandi, Mdumba, Misyaje, Mbesa, Uliwana, Chukano, Nasumba, Wenje, Mkapande, Nuwemecho, Nasya, Namasadau, Miseula, Ligoma, Chemchem, Makade, Kozango, Likada, Senei, Azimio, Angalia na kadhalika. Tunaiomba Serikali kutuchimbia visima virefu na vifupi ili kutoa huduma ya maji safi kwa wananchi wa Jimbo la Tunduru Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi ya maji miwili ya Mbesi na Mtina ni ya muda mrefu bado inasuasua katika ukamilishaji wake na mradi wa Mtina Mkataba wa ujenzi Halmashauri umekatishwa wakati mradi umefikiwa zaidi ya asilimia 60, kufanya mradi ule uendelee kuchelewa zaidi kukamilika. Vile vile tunaomba miradi mipya ya maji ili kupunguza adha ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la elimu. Upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa na vyoo pamoja na nyumba za Walimu. Kuna tatizo kubwa sana la vyumba vya madarasa kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi katika shule za msingi, hivyo tunaomba Serikali isaidie kutoa fedha kuongeza jitihada zilizofanywa na wananchi ambao wanaweza kufyatua tofali 100,000 kwa ajili ya madarasa na nyumba za Walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Tunduru Kusini halina high school hata moja, tumeomba angalau shule mbili za Kata zipandishwe hadhi ili ziwe high school.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kuchangia hoja ya hotuba ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgao wa Wilaya, Wilaya ya Tunduru ina eneo kubwa sana la utawala kulinganisha na eneo la Mkoa wa Mtwara wenye Wilaya sita. Tunaomba Serikali ifikirie suala la kugawa Wilaya ya Tunduru ili kurahisisha shughuli za kuhudumia wananchi kwa kuleta huduma karibu na wananchi. Kila eneo la jimbo liwe Wilaya kamili inayojitegemea kutokana na wingi wa watu na umbali kutoka Makao Makuu ya Wilaya ilipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la watumishi wa halmashauri; tuna upungufu mkubwa wa watumishi wa halmashauri katika sekta zote za afya, elimu na kada zingine za kilimo. Tuna upungufu wa Walimu wa shule za msingi zaidi ya 1,000 na Walimu wa sayansi shule za sekondari zaidi ya 100 na kuna upungufu wa watumishi wa afya zaidi ya 700, tuna watumishi asilimia 26 tu katika sekta ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watumishi wa halmashauri wamekaa muda mrefu katika Halmashauri ya Tunduru na wanasababisha kudumaa kwa kazi za halmashauri na wanafanya kazi kwa mazoea. Hivyo, tunaomba watumishi waliokaa muda mrefu wahamishwe wapelekwe halmashauri zingine ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vituo vya afya, halmashauri ya Tunduru ina kata 35 ina vituo vya afya vitano tu. Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga Kituo cha Afya Nalasi lakini mpaka leo kuna msingi tu. Wananchi walifyatua tofali za udongo lakini tangu 2014 mpaka leo hamna kinachoendelea. Halmashauri imetenga fedha kila mwaka lakini hazipatikani kabisa, hivyo naomba Kituo hicho cha Afya Nalasi ambacho kitahudumia Kata za Nalasi Magharibi na Nalasi Mashariki zenye wakazi zaidi ya 30,000 kujengwa na Serikali ili kuheshimu ahadi ya Rais Awamu ya Nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambasamba na kituo hicho naomba Serikali isaidie halmashauri kujenga vituo vya afya angalau vinne zaidi kupunguza adha ya huduma kwa akinamama na watoto. Kata hizo ni Malumba, Lukumbule, Ligoma, Msechela na Tuwemacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa la maji katika maeneo mengi ya Jimbo la Tunduru Kusini. Kutokana na mabadiliko ya tabianchi mito mingi imekauka kabisa hasa katika Vijiji vya Mchoteka, Likweso, Mnemasi, Molandi, Machemba, Misyaje, Mbesa, Chiwana, Chikomo, Nasomba, Wenje, Mkapunda, Tuwemacho, Nasya, Namasalau, Misechela, Ligoma Chemchem, Mkandu, Kazamoyo, Lukala, Semeni, Azimio, Angalia na kadhalika. Tunaiomba Serikali kutuchimbia visima virefu na vifupi ili kutoa huduma ya maji kwa wananchi wa Jimbo la Tunduru Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi ya maji miwili ya Mbesa na Mtina ni ya muda mrefu bado inasuasua katika ukamilishaji wake. Mradi wa Mtina mkataba wa ujenzi halmashauri umekatishwa wakati mradi umefikia zaidi ya asilimia 60 na kufanya mradi ule kuchelewa zaidi kukamilika. Vilevile tunaomba miradi mipya ya maji ili kupunguza adha ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la elimu, kuna upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa na vyoo pamoja na nyumba za Walimu. Kuna tatizo kubwa sana la vyumba vya madarasa kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi katika shule za msingi, hivyo, tunaomba Serikali isaidie kutoa fedha kuongeza jitihada zilizofanywa na wananchi ambao wameweza kufyatua matofali 100,000 katika kila kijiji kwa ajili ya kujenga vyoo, madarasa na nyumba za Walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, Jimbo la Tunduru Kusini hamna shule ya high school hata moja. Tunaomba angalau shule mbili za kata zipandishwe hadhi ili ziwe high school.