Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa dakika hizi tano. Moja kwa moja naenda kwenye hiki kitabu cha TAMISEMI, ukurasa wa 12 - 13 katika masuala ya utawala bora inaonesha kwamba Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Maafisa Utumishi na Mipango pamoja na Makatibu Tawala wamepewa mafunzo kuhusu utawala bora. Sasa sielewi hayo mafunzo waliyowapa yalikuwa yanahusu nini? (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utawala bora kuna misingi. Misingi ya utawala bora moja ni utawala wa sheria (rule of law), waliwafundisha nini? Katika misingi ya utawala bora ninachojua mimi uwajibikaji in English (accountability), waliwafundisha nini? Katika misingi ya utawala bora uwazi katika uongozi yaani Bunge, Mahakama, vyombo vya maamuzi, transparent in English, waliwafundisha nini? Katika misingi ya utawala bora uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa watu kutoa mawazo yao bila vitisho. Sasa tukiangalia nchi yetu hivi sasa hivi kuna utawala bora ama bora utawala? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa Wakuu wa Mikoa wame-prove failure. Wakuu wa Wilaya baadhi yao na Wakuu wa Mikoa wameonesha hawajafaulu huo mtihani wamepoteza hela za Serikali za kodi za wananchi kwa kuwapa mafunzo halafu wakienda kule hawafanyi walichojifunza. Labda wangeniita mimi mwenyewe ni Mwalimu wa utawala bora vilevile na maendeleo ya uchumi nije nitoe mada halafu wangepewa mitihani huko field, wale wanaofeli wanawatoa katika uongozi.

T A A R I F A . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano Mkuu wa Mkoa wa Morogoro safari hii kafanya maajabu, Dkt. Kebwe tena alikuwa Mbunge huku, eti leo hajaitisha RCC, hajaitisha Road Board, vitabu kaleta TAMISEMI, huo ndiyo utawala bora? Wabunge hatujahusishwa katika mipango yetu ya Mkoa wa Morogoro, mkoa mkubwa, hivi kwa nini wanamkabidhi mtu kama yule mkoa mkubwa kama ule? Wananiambia ukisema
ndiyo watamwacha pale pale, muacheni lakini CCM inaenda kuondoka, mimi nawaambia, anaenda kuwadondosha jumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani mkoa mkubwa kama Morogoro na tulikwishaomba jamani mtupunguzie huu mkoa, mtupe Mkoa wa Kilombero mpaka leo hamna kitu. Tutaona kwenye bajeti hii, kuna majimbo wamewapa hela kama mkoa ndiyo tutakuja kushughulika na ninyi. Sisi Mkoa wa Morogoro mkoa mkubwa hamna chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja Mlimba sasa. Mlimba halafu Mheshimiwa Jafo alipokuwa Naibu Waziri…

T A A R I F A . . .

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba muda wangu ulindwe dakika zenyewe ni tano tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mlimba, Mheshimiwa Jafo aliniahidi atakuja Mlimba ndugu yangu mpaka leo Mlimba hawajaja wanataka nini? Kwa nini hawaji Mlimba kuangalia wakija wanaishia Ifakara na Morogoro, Mlimba ni hatari. Hivi ninavyozungumza barabara karibuni, nawashukuru TANROAD kidogo wanajitahidi kutengeneza tengeneza barabara lakini barabara imekuwa ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Mawaziri, Waziri wa TAMISEMI mimi siwezi kusema sana hapa nawaomba waje Mlimba. Kwa mfano, tulikuwa tunategemea mwaka huu tutapata hela katika Kituo cha Afya cha Mngeta, cha Mchombe lakini hamna hata shilingi. Kilometa 265 mpaka kwenda kwenye hospitali ya wilaya akinamama wajawazito wanakufa njiani jamani, watoto wanakufa, tatizo ni nini? Kwa nini hawaji wakaangalia mazingira halafu waone maeneo ambayo yalikuwa muda mrefu hayana huduma ili watuletee hizo huduma angalau, barabara tukose….

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)