Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia. Nianze kwa kumpongeza Waziri wa TAMISEMI pamoja na Naibu wake. Mheshimiwa Waziri ninachoweza kusema kuhusu yeye ni kusema tu yeye ni mzalendo. Vile vile nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipa Wizara yake Katibu Mkuu mahiri, Mzee wetu Iyombe pamoja na wasaidizi wake ambao wanafanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nianze kwa kuishukuru Serikali kwa niaba ya watu wa Siha kwa ajili ya shilingi bilioni 52 za barabara, shilingi bilioni mbili kwa ajili ya hospitali ya wilaya, shilingi milioni 700 kwa ajili ya Zahanati ya Umakiwaru, shilingi milioni 680 kwa ajili ya kumalizia miradi ambayo ilikuwa haijamaliziwa, shilingi bilioni 2.8 kwa ajili ya maji na shilingi milioni 931 kwa ajili ya daraja. Hiyo nimesema ili watu wajue kwamba watu wa Siha hawakukurupuka, walijua wanafanya nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini watu wetu mwaka huu wameotesha kuanzia mwezi wa Nne na wengine sasa wanalima kwa juhudi sana kwa ajili ya kuzalisha. Kama watu wetu wanafanya hivyo ni muhimu sana Wizara husika kuanzia sasa kwa sababu tunataka tunyanyue uchumi wa watu wetu basi waanze kutafakari ni namna gani kilimo ambacho wanakifanya watu wetu sasa hivi kitakuwa na tija watakapofikia wakati wa mavuno. Kwa sababu imekuwa ni utaratibu wa kawaida kwamba inapofika wakati wa mavuno na mauzo mahindi yanafungwa na mipaka inafungwa ili wasiuze nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri tutafakari namna mpya ya kufanya hilo kwa sababu kwa muda mrefu unaweza ukafikiri unadhibiti mfumuko wa bei kwa kuzuia mahindi yasiende nje, lakini kwa muda mwingine unaweza ukasababisha wananchi wakaacha kuzalisha mazao ya chakula wakaanza kuzalisha mazao mbadala. Matokeo yake hata ile bei ya mazao tuliyofikiri tunaidhibiti ikapanda na ikawa tu umefanya kazi ya muda mfupi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile soko la mbaazi. Nafikiri ni mapema sasa tuanze kushughulika na soko la mbaazi. Tumeambiwa kwamba nchi ya India ndiyo imekuwa ikinunua mazao yetu ya mbaazi, ni vizuri kwa sababu na sisi tunanunua dawa kutoka kwao tuanze kuzungumza sisi tunachukua dawa kwenu nyingi kwa ajili ya watu wetu na nyie mnachukuaje mbaazi yetu na tunaanza kujadili kuanzia hapo ili tuweze kufanya biashara yenye tija kwa ajili ya wakulima wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwenye Wilaya yangu ya Siha kuna ardhi kubwa sana, kuna ardhi ya NARCO zaidi ya heka 56,000 na ya TALIRI zaidi ya heka 14,000. TALIRI na NARCO wana ng’ombe kidogo sana na TALIRI wanafanya research ya mifugo bora lakini utaona NARCO wanataka kufuga mifugo waanze kuwa wachungaji. Nashauri TALIRI wafanye research ya mifugo na wazalishe mifugo mizuri sana, NARCO wafuge hiyo mifugo lakini wajenge kiwanda ndani ya NARCO na ile mifugo mizuri wapewe wafugaji wetu waweze kuzalisha mifugo na kiwanda ambacho kitakuwa pale Siha kiweze kutumika kwa ajili ya kuvuna hiyo mifugo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo niende kwenye eneo la utawala bora. Nimesikia rafiki zangu wengi wamekuwa wakiongea na kukosoa kuhusu utawala bora, lakini utawala bora unaanzia kwenye nyumba yako. Namshukuru rafiki yangu Mheshimiwa Lusinde leo ameanza vizuri kwenye kuelezea eneo moja lakini nimesikia habari moja ikisema kwamba Mheshimiwa Lusinde hajasoma kitabu kizima. Naomba nitoe mifano ambayo haihitaji usome kitabu kizima ili uelewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge walioko hapa kuna Wabunge wanachangishwa zaidi ya Sh.500,000/= na wengine wanachangishwa zaidi ya Sh.1,500,000/= na ukipiga hesabu kwa mwezi mmoja ni zaidi ya Sh.73,000,000/= kwa mwaka mzima ni zaidi ya Sh.876,000,000/=. Nilisema juzi kidogo kelele nyingi zikapigwa lakini nikawa najiuliza Wabunge hawa leo wanakosa nafasi ya kufanya siasa kwenye Bunge hili kwa sababu imekosekana kuajiriwa tu wafanyakazi wanne lakini Wabunge hawa wamechumwa zaidi ya shilingi milioni 876. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua umuhimu wa wao kuhitaji watumishi hao…

TAARIFA . . .

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakubali kabisa sihitajiki kuingilia mipango ya chama chochote, lakini ukweli tu ni mmoja kwamba ni logic ya kawaida kama unapata milioni isiyozidi 460 kwa mwezi na unashindwa hata kuweka programu ya ndani ya nyumba yako vizuri…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizomea na wengine wakipiga makofi)

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu unamtaka Dokta Mollel apambane na wewe ili uweze kutimiza azma yako ya …

(Hapa baadhi ya Wabunge walizomea na wengine walipiga makofi)

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, unataka Dokta Mollel ashirikiane na wewe ili muweze kumiliki Benki Kuu, wazalendo kama sisi hatuwezi kuwakabidhi Benki Kuu kama milioni 400 hamuwezi kusimamia. (Makofi)

Mwenyekiti, lakini nimwambie dada yangu kwamba mimi namtetea kwa sababu Wabunge wa Majimbo wanachangishwa Sh.500,000/= na Viti Maalum wanachangishwa Sh.1,500,000/=

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme hapa tunazungumzia suala la utawala bora na watu wamekuwa wakitoka mapovu kwa ajili ya kujitahidi kuonesha kwamba Serikali iliyoko madarakani imeshindwa kujipanga na kuendesha mambo na wakijionesha kwamba wao ni Serikali inayotakiwa kuja kuwa Serikali mbadala kwa ajili ya nchi hii, lakini imeshindwa kusimamia milioni hizo nilizozitaja, basi kuna sababu kubwa ya kusema Watanzania wasiwaamini na hawana uwezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaweza ukafikiri shilingi bilioni mbili alizozitaja Mheshimiwa Lusinde hapa ni nyingi, ni nyingi kuliko zilizoko Serikalini kwa sababu ndiyo hela pekee walizokuwanazo. Kwa hiyo, hela 100% zimeenda mikono…

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kuzungumzia suala la usalama. Vilevile limekuwa likizungumzwa suala la usalama kwenye Bunge hili, usalama sio suala la tu la vyombo vyetu vya usalama peke yake vilevile ni suala la watu wote na viongozi wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kuna kikundi kidogo ambacho kimekuwa kiki-remote watu ambao wanapiga kelele hapa wasiojua wanachokifanya baada ya mirija yao kufungwa na wamekuwa wakitaka ku-propagate kwamba kuna usalama na wao wenyewe wakitumia…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizomea na wengine walipiga makofi)