Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iangalie upya utaratibu wa pembejeo za ruzuku kama (wanufaika) walengwa hawanufaiki na mfumo wa sasa ambao mawakala wanawauzia wakulima mbolea kwa bei ya juu kuliko bei ya soko kwa maeneo ya vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, zao la viazi mviringo ni zao la kiuchumi kwa wananchi wa Jimbo la Njombe Mjini na Mkoa mzima wa Njombe katika msimu wa Machi mwaka huu. Viazi vimeathirika na ugonjwa ambao hadi leo haujafahamika vizuri. Sasa niiombe Serikali ifanye utafiti na kuwaelimisha wananchi ili waweze kujizatiti na msimu mwingine. Pia Serikali iangalie jinsi inavyoweza kusaidia mbegu mpya ya viazi kwa wananchi wa Jimbo la Njombe Mjini ili kuwasaidia wakulima kwanza katika uzalishaji wa viazi vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Benki ya Kilimo; naipongeza Serikali kwa kuanzisha Benki ya Kilimo, benki hii iongezewe mtaji ili iweze kukopesha wakulima wengi zaidi. Benki hii ianzishe dirisha la mikopo kwa wakulima wa kati ili kusaidia kasi ya kilimo na kuongeza ajira kwa haraka, kuliko sasa inapojihusisha zaidi na wakulima waliopo kwenye vikundi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Benki hii ifungue tawi Njombe kwani ipo katikati ya Mikoa ya Iringa, Ruvuma na Mbeya na Mikoa hii shughuli kubwa ya wananchi ni kilimo cha mazao ya chakula, hivyo itakuwa imejiweka katika mazingira ambayo yatawezesha huduma kwa wakulima wengi zaidi na kuwapunguzia gharama ya kusafiri hadi Dar es Salaam. Pia hata benki yenyewe itakuwa rahisi kuwatembelea wakulima. Haya yote mwisho wa siku yanaongeza tija na kupunguza gharama kwa wakulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.