Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kutoa pole kwa changamoto ambazo viongozi wa kisiasa wa CHADEMA wanapitia. Muda nilionao ni dakika tano, sitaongea mengi, lakini natoa pole sana na ninaamini katika dhana ya utawala bora watu wengi wanaweza kuongea na wanaelewa nini maana ya utawala bora kama tuna viongozi na Wabunge zaidi ya 15 wa Vyama vya Upinzani wanatakiwa kuripoti polisi karibu kila wiki. Salamu zimefika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nataka nishangae Wizara na utamaduni mpya walioanzisha wa kujibu eti hotuba ya CAG. Nitaongelea TAMISEMI, mfano waliojibu jana na wakatoa taarifa kwamba mapendekezo aliyoyatoa CAG wameyafanyia kazi ikiwa ni pamoja na kufukuza watumishi takribani 4000 na nimei-quote vizuri ambao walituhumiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie kwa mujibu wa CAG kwenye report aliyoitoa kuna mapendekezo aliyatoa mwaka 2000. Katika kalenda hii ya mwaka 2014/2015 alitoa mapendekezo 15 lakini mpaka mwaka 2017 mapendekezo yenyewe 14 yalikuwa hayajafanyiwa kazi. Kuanzia mwaka 2014/2015 mpaka 2017 aliyoyatoa juzi ndiyo mnaanza kuyajibu kwenye television. Inashangaza sana. Ninachoweza kuwaambia, nendeni mkafanyie kazi mapendekezo aliyoyatoa na siyo kwenda kujibu kwenye television. Mna kazi kubwa ya kufanya, nendeni mkaangalie upungufu aliouainisha kwenye Wizara zenu, kwenye Serikali za Mitaa ili mtuletee majibu sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni kusikitika kwa kuambiwa makusanyo ya Serikali yanapanda kwa asilimia 90 huku Halmashauri zetu mpaka mwezi wa sita mwaka 2017 zikiwa zimepelekewa asilimia 49 tu ya fedha zilizohitajika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ina upungufu wa asilimia 68; Halmashauri ya Kibondo upungufu wa asilimia 88 na Halmashauri ya Kigamboni, upungufu wa asilimia 86. Halafu tunakuja humu Wabunge wenzangu wa CCM mnapongeza. Halmashauri zetu zimepelekewa asilimia 49 tu ya fedha za maendeleo. Tutabaki kusifiana hapa, lakini mwisho wa siku tutaona aibu sisi wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nitaliongelea ni Wakuu wa Wilaya kukosa instruments. Hii nai- associate na kazi wanayoifanya Wakuu wa Wilaya na Mikoa, wanawakilisha wanaliowatuma. Tumeona mfano mdogo au mfano mkubwa niseme, anachokifanya Mkuu wa Mkoa wa sasa aliyepandishwa, baada ya kutumiwa na CHADEMA kununua Madiwani, akapandishwa kuwa Mkuu wa Mkoa. Sasa ameenda mbali zaidi, anajitangaza hadharani kwamba atawabagua watu wa CHADEMA, atawabagua watu wa upinzani kwa sababu yeye anafanya kazi kwa Ilani ya CCM na hawezi kufanyakazi kwa Ilani ya CHADEMA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami napigia msitari, kwa vile anamwakilisha mtu fulani ambaye ni Rais, kauli ya Mkuu wa Wilaya au kauli ya Mkuu wa Mkoa ni kauli ya Mheshimiwa Rais, kwa hiyo, na sisi tunaweza kusema na hiyo ni kauli ya Rais unless kuwepo na kanusho la kauli aliyoitoa Mnyeti kwamba atazidi kuwabagua wapinzani katika maeneo anayoyaongoza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa mbalimbali za fedha kwa mujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali zimeonesha upungufu mkubwa sana, mfano, Halmashauri ya Bukoba Mjini ilikuwa na takribani shilingi milioni 60 kwenye madaftari, lakini fedha haijapalekwa benki. Halmashauri ya Kigoma-Ujiji ina zaidi ya shilingi milioni 219 katika daftari, lakini fedha hazijapelekwa benki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo inaonesha upungufu mkubwa sana na tunakimbilia kujibu kwenye magazeti, nadhani twende kwenye Halmashauri husika tuone chamgamoto ni ipi? Tufanyie kazi mapendekezo yanayotolewa na CAG, vinginevyo hatuna haja ya ku- allocate fedha kwa CAG kama mapendekezo hatuwezi kuyafanyia kazi, tunakwenda kuwajibu waandishi wa habari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala kubwa kama nitafanikiwa kulimazilia ni kutotengwa kwa asilimia 10 kwa ajili ya wanawake na vijana kwenye Halmashauri. Nimesikia Mheshimiwa Waziri mmoja hapa akisema na zile asilimia 10 zitakuwa hazitolewi riba, lakini kwa mujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali anaonesha takribani Halmashauri 164 hazijatenga asilimia hiyo 10 kwenda kwa vijana na akina mama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sijui mnavyosema kwamba mnaondoa riba, mnaondoa katika kitu ambacho hakipo? Ni lazima tukae vizuri, tujipange. Kama kweli TAMISEMI iko serious inataka Halmashauri zitenge hiyo fedha, iandae account maalum katika kila kiasi kitakachokusanywa, basi hiyo asilimia ipelekwe.