Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ningependa kutumia nafasi hii kuainisha upungufu unaofanywa na baadhi ya Jeshi la Polisi. Polisi kazi yao ni kulinda wananchi na mali zao, mipaka ya nchi na pia kuhakikisha amani inapatikana. Pia kudhibiti uhalifu wowote unaoweza kutokea ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kwa sasa imekuwa ni kinyume na hayo, Jeshi letu la Polisi limepoteza uaminifu kwa wananchi wake kutokana na vitendo wanavyofanya. Kwa mfano, wananchi kubambikiwa kesi awapo kituoni. Unakuta mtu ana kesi ya kupiga mwenzake anaambiwa ameiba na kuvunja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuzuia mikutano ya vyama vya siasa kinyume na taratibu ya Katiba ya nchi. Hivyo ningeomba Waziri mwenye dhamana aelekeze Jeshi la Polisi majukumu yao halisi na siyo vitendo vya uonevu wanavyovifanya sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Askari wanapenda rushwa na kuchelewesha kesi Mahakamani sababu wanachopewa hakiendani na kazi wanazofanya. Hivyo naomba waongezewe mishahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia na makazi ya baadhi ya askari nchini hayaridhishi na yanaenda kinyume na mila na desturi ya nchi yetu. Unakuta mtu anaishi kwenye chumba kimoja na ana familia, chumba kinatenganishwa na pazia au ma-box. Je, hayo ni maadili gani? Hao askari wanatembelewa na ndugu zao, uhuru hawaupati kabisa. Namwomba Waziri, Mheshimiwa Mwigulu jambo hili litazamwe kwa makini japo wakirudi majumbani kwao kupumzika wapumzike vizuri ili wakirudi kazini warudi na nguvu nzuri.