Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Mwigulu L. Nchemba kwa kuwasilisha bajeti ya Wizara yake katika kipindi cha bajeti cha 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze Wizara hii kwa kazi kubwa wanazozifanya katika kuendelea kudhibiti vitendo vibaya, viovu vinavyofanyika katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana Wajumbe wa Kamati kwa kufanya ziara katika Mkoa wa Lindi. Kwa kweli wamethibitisha uchakavu wa nyumba za maaskari wetu zilivyochakaa, inatia huruma sana. Naiomba sana Serikali katika nyumba hizi zitakazojengwa katika kipindi cha bajeti hii ya 2018/2019, tupate mgao wa nyumba kwa ajili ya Polisi wetu na Askari Magereza katika Wilaya za Lindi Manispaa na Wilaya ya Nachingwea; naiomba Serikali kusikia kilio chetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kuunga mkono hoja.