Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kunijalia uhai hadi kuona siku hii ya leo. Jeshi la Polisi ni taasisi muhimu kwa ajili ya ulinzi wa raia na mali zao. Jeshi hili liachwe huru kabisa lifanye kazi yake kwa mujibu wa taratibu na sheria zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi lisitumike kisiasa na watawala wote waache kutoa maagizo kwa jeshi hili lifanye kwa matakwa yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakuu wa Wilaya wanapofanya ziara zao vijijini wanaandamana na magari ya polisi kiasi cha kuwatia wananchi hofu. Mbona sisi Wabunge tunafanya ziara bila polisi na usalama upo wa kutosha? Kutembea na mapolisi ni matumizi mabaya ya Jeshi hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kuhusu vitambulisho vya uraia (NIDA). Mradi huu ulitengewa fedha za kutosha lakini wakati wa utekelezaji wake wananchi wetu katika Wilaya ya Karatu walichangishwa fedha kwa kila mmoja Sh.1,000/= kama sharti la kupata kitambulisho. Kwa nini wananchi wachangishwe wakati Serikali ilitoa fedha kwa mradi huu? Naomba kupatiwa ufafanuzi wa jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Karatu ilitoa ardhi eneo la Njiapanda (Bashay) ekari 60 kwa Jeshi la Magereza ili kujenga Magereza ya Wilaya ya Karatu. Hadi leo bado magereza hayo hayajajengwa. Jeshi la Magereza kama halihitaji lirudishe eneo hilo kwa halmashauri.