Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, namshukuru Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchimba, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa hotuba yake nzuri, lakini naomba kutoa ushauri kama ifuatavyo:-

(i) Serikali ifunge vifaa vya kudhibiti mwendo katika magari ya mizigo (malori) maana mara nyingi husababisha ajali.

(ii) Ili kuondoa sitofahamu kwa Watanzania, Kitengo cha Madawa ya Kulevya pindi wanapoteketeza madawa hayo mfano cocaine na heroine ioneshe hadharani kama wanavyoonesha bangi.

(iii) Serikali iharakishe upelelezi katika kesi zinazowakabili wananchi. Upelelezi uwe unafanywa kwa haraka ili kuepusha mlundikano wa kesi na mlundikano wa mahabusu katika magereza yetu.

(iv) Kikosi cha Zimamoto hususan Mkoa wa Dar es Salaam kimebuni mradi wa kuwauzia wafanyabiashara vifaa vya kuzimia moto (fire extinguishers). Hii hupelekea kuongezeka kwa utitiri wa kodi kwa wafanyabiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wawaendee wenye nyumba (wamiliki wa majengo) wanununue fire extinguisher waweke katika corridors za majengo na siyo ndani ya maduka. Maana wakati mwingine moto hutokea nyakati za usiku wakati mmiliki wa duka yupo nyumbani amelala. Kwa hiyo, fire extinguisher haina msaada wowote maana ipo ndani ya maduka siyo nje katika corridor.

(v) Askari wa usalama barabarani (traffic) ni kero sana kwa watumiaji wa vyombo vya moto. Mara nyingi kuna makosa mengine askari wa usalama barabarani anapaswa kumwelimisha anayeendesha chombo cha moto na siyo kosa la kutoza faini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali halisi inaonesha kabisa wapo barabarani kuisaidia Serikali kukusanya mapato ya nchi na siyo kuelimisha jamii au madereva katika kulinda usalama wao na mali zao. Serikali itoe semina kwa askari wa usalama barabarani ili wawe na weledi na kujua majukumu yao na siyo kuleta kero kwa watumiaji wa vyombo vya moto.

(vi) Kuna baadhi ya askari wetu wamepandishwa vyeo lakini mishahara yao haijapandishwa. Suala la kupandishwa cheo kwa askari liende sambamba na kuongezwa mishahara.

(vii) Serikali ipunguze gharama za kupata passport ya Sh.150,000 maana ni ghali mno ukizingatia kipato au kima cha chini cha Mtanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, namwombea Mheshimiwa Waziri kila la kheri na Mungu ampe umri mrefu na afya njema katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.