Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu muumba mbingu na ardhi, mwingi wa rehema. Pia nakushukuru kwa kupata fursa hii ya kuchangia kwa maandishi hoja iliyopo mezani sasa. Napenda kuzungumzia Vitambulisho vya Uraia; pigwapigwa inayofanywa Zanzibar na Vikosi vya SMZ wakati huohuo Polisi wanawalinda wapigaji na kuwekwa ndani Mashekhe kwa kipindi kirefu bila kujali sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na vitambulisho. Kuhusu suala hili japo halijakaa sawa kabisa, bado kuna Watanzania wengi hawajapatiwa vitambulisho ilhali tayari wameshatimia umri wa miaka 18.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pigapiga inayofanywa kule Zanzibar na Vikosi vya SMZ inatisha. Baya zaidi Askari Polisi ambao wao ndiyo wenye dhamana ya kulinda raia na mali zao huwa wao Polisi wanawalinda hawa wapigaji ambao ni Vikosi vya SMZ. Kama kuna makosa yoyote yanayofanywa kwa mujibu wa sheria basi watu hawa wapelekwe Mahakamani. Haya wanayoyafanya Vikosi vya SMZ hawana mamlaka ya kuyafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Zanzibar limekuwa ni jambo la kawaida kupigwa, kutekwa, kupotezwa na hata kutupwa vichakani. Baya zaidi kuna mtu amepigwa nyumbani kwake usiku na Polisi na baadaye akakimbizwa hospitali na baada ya siku kama ya tatu mzee yule akafariki. Tunakwenda wapi Watanzania?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie kuhusu Mashekhe waliowekwa ndani kwa miaka kadhaa sasa. Hivi ni upelelezi wa aina gani hadi leo ushahidi haujakamilika? Inashangaza sana. Wabakaji, wahuni, walawiti watoto, wote hawa ushahidi umethibitika lakini kwa Mashekhe ambao kimsingi hawana makosa yoyote mpaka leo bado.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.