Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Waziri na Naibu Waziri wake. Ningependa kuchangia kuhusu suala la mbegu za mahindi zinazotumika kwa sasa, ningependekeza utafiti ufanyike ili tuweze kupata mbegu mpya. Kwani ni mbegu ambazo zinatumika sasa ni za muda mrefu zimechoka sana. Ukilima ekari moja unategemea kupata gunia siyo chini ya gunia 35, lakini mbegu hii iliyopo ukipata gunia nne ni bahati. Hivyo ni vema Serikali ikafanya utafiti kutumia vyuo vyetu ili tupate mbegu bora. „Kama ukitaka mali utaipata shambani’.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishauri suala la umwagiliaji litiliwe kipaumbele kwani tumeshuhudia mwaka huu mvua nyingi zimenyesha lakini sikuona jitihada za Serikali na hasa Wizara yako na Wizara ya Maji kuweza kuvuna maji ambayo tumeshuhudia maji mengi yakipotea bure.
Mheshimiwa Waziri hata suala la migogoro ya wakulima na wafugaji, tatizo siyo ardhi tatizo ni utengaji wa maeneo ya mifugo kupata sehemu ya kwenda kunywa maji. Hivyo endapo itatenga na kujenga mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji na sehemu ya kunyweshea mifugo suala hili la migogoro ya wafugaji na wakulima litapungua sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ningeomba sana Wizara ya Kilimo, iweze kumsaidia mkulima itabidi Wizara yake kushirikiana na wadau kuona jinsi ya kumaliza suala la Lumbesa, wakulima wanapata tabu sana.