Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Rose Kamili Sukum

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea ukurasa wa kumi wa hotuba ya Waziri kuhusu ujenzi na ukarabati wa nyumba za polisi. Tunapenda kujua kati ya nyumba 400 zinazotarajiwa kujengwa kama Vituo yya Polisi Bassotu na Endasak vinahusika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kama fedha zilizotolewa za maendeleo kiasi cha Sh.38,285,682,000/= zinahusiana na ujenzi na ukarabati wa nyumba za polisi. Kama ndivyo, je, Vituo vya Polisi katika Wilaya ya Hanang, Mkoani Manyara vina kiasi gani cha fedha za ujenzi na ukarabati? Wakati Mheshimiwa Waziri anajibu hoja, naomba kujua kama Vituo vya Polisi Bassotu na Endasaki vimetengewa fedha, kwani Kituo cha Bassotu Wilayani Hanang Mkoani Manyara, wamepewa barua ya kuondoka katika nyumba ambayo waliomba kuishi kwa muda kama kituo cha polisi. Je, lini kituo hicho kitajengwa na nyumba za polisi kwa ajili ya usalama wa raia na mali zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni usafiri. Kutokana na kuwa na eneo kubwa la ulinzi kunatakiwa usafiri wa uhakika kwa polisi wetu wanaoishi kwenye vituo ambavyo vipo pembezoni na mbali na makao makuu ya Polisi Wilaya. Kwa hiyo, naomba kupatikane gari ambalo litawasaidia Polisi Bassotu ili waweze kulinda wananchi, raia na mali zao kwa urahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni ajira. Naomba askari wa kutosha wa kike ili kuhifadhi hadhi ya wanawake kwani wanawake ni wengi sana kuliko wanaume.