Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji Wakuu kwa kazi kubwa ya kutunza amani nchini, Mheshimiwa Waziri hongera sana na ni ukweli usiopingika kwmba, kazi nzuri inafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nalipongeza Jeshi la Polisi hasa Dawati la Jinsia kwa kazi nzuri wanayofanya, limekuwa kimbilio la wanyonge na wenye manyanyaso mbalimbali. Dawati hili lilitoa takwimu juu ya ukatili majumbani, wanawake wanaoteswa, wanaopigwa, kubakwa na kuuawa zinatisha lakini takwimu za watoto wanaoteswa, wanaolawitiwa/kubakwa ni kubwa mno. Napenda kujua Wizara ina mpango gani ili kudhibiti ukatili mkubwa wanaofanyiwa wanawake na watoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila siku wanakamatwa wahamiaji haramu wanaoingia nchini kinyume na utaratibu. Hawa watu wanaweza kuingia na kuingiza silaha kitu kinachohatarisha usalama wa nchi yetu. Najua mipaka yetu iko porous, napenda kujua Jeshi la Polisi/Wizara wana mpango gani wa kudhibiti uingizaji wa silaha kupitia mipaka yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.