Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya usalama katika nchi yetu ni tete. Watu wengi wamekuwa wakitekwa na kuuawa na hata wengine wanauawa na Polisi kama vile Suguta Chacha, mdogo wake Mbunge mwenzetu, ameuawa na Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli hali hii inaharibu kabisa hali ya amani na utulivu. Naiomba Serikali mchukue mkakati wa makusudi kuhakikisha mnakomesha hali hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya Wabunge, hasa Wabunge wa Upinzani, wamekuwa wakizuiwa kufanya mikutano. Polisi wamekuwa wakiwaandikia barua ya kuwazuia wasifanye mikutano. Hii siyo sahihi kabisa. Huko ni kukiuka Katiba ya nchi yetu. Naiomba Serikali ichukue hatua ya makusudi kuhakikisha inatenda haki kwa watu wetu na hasa kuwaruhusu Waheshimiwa Wabunge wafanye mikutano kama Katiba inavyodai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi wa barabarani wanafanya kazi ya TRA, wanasumbua sana madereva. Madereva wananyanyasika, kulipa faini kila Kituo cha Polisi, pia kama hawana pesa za rushwa wananyang’anywa kadi za gari na leseni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali iwasaidie vijana wetu wanaoendesha bajaji, bodaboda na magari madogo ya mizigo; wanatozwa pesa bila sababu. Naomba Serikali isimamie Polisi wa Usalama Barabarani wasiwapige viboko madereva. Huo kwa kweli ni uonevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali iache kutumia Polisi kwa kuwadhalilisha Wabunge wa Upinzani kwa kuwakamata kamata ovyo, hata kuwapiga makofi, mfano, Mheshimiwa Susan Kiwanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.