Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kwa kuyasema mambo matatu muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi Mchinga, bado kina changamoto nyingi ingawa kimekitajwa katika ukurasa wa kumi wa kitabu cha hotuba. Kituo kile kimejengwa tangu mwaka 2002, lakini hadi leo bado hakijakamilika; Askari wamehamia pale lakini hawana nyumba hata moja ya kuishi. Hivyo wanaishi Lindi Mjini na wanalazimika kuja asubuhi na jioni kurudi Lindi. inapofika wakati wa usiku ikitokea dharura ya kuhitajika huduma za Kipolisi wananchi hawawezi kupata huduma hiyo. Naomba Ofisi ya Mheshimiwa Waziri itenge fedha za angalau nyumba tatu za kuishi Askari pale Mchinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kuhusu Kituo cha Polisi Rutamba. Kituo hiki pia kipo Jimbo la Mchinga. Kituo hiki kinakabiliwa na changamoto kubwa ya makazi ya Askari, hakuna nyumba za makazi ya Polisi, lakini pia jengo lenyewe la kituo limechakaa na halikidhi haja ya kuwa Kituo cha Polisi. Naomba watutengee pesa za kujenga jengo la Kituo cha Polisi Rutamba pamoja na nyumba za Askari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ni kwamba, magari ya Polisi Lindi (Wilaya) yote yamechakaa, hivyo yanaharibika mara kwa mara. Askari Polisi hamwapi OC, hivyo mara kwa mara wamekuwa wakitusumbua sisi Wabunge tuwape fedha za matengenezo ya magari yao pamoja na mafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namuuliza Mheshimiwa Waziri, kwa nini wanawatesa hivi Askari na kulidhalilisha Jeshi wakiacha mafao yao ambayo bado machache? Hata magari yao ya kufanyia kazi nayo ni shida pia. Waone aibu, watengeneze magari ya Askari, ya Ofisi ya OCD Lindi pamoja na kupewa mafuta yatakayowezesha kutekeleza majukumu yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni hayo tu.