Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na ukiukwaji wa haki za raia wa Mkoa wa Kigoma na kusumbuliwa kuwa siyo raia wa Tanzania. Kakonko kila basi linasimamishwa na kukaguliwa na Maafisa wa Uhamiaji. Abiria wanavuliwa nguo za juu, yaani t-shirt au blauzi ili kuona chanjo iko mkono gani kulia au kushoto? Huu ni udhalilishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanachukua rushwa kwa kila raia atakayekosa kitambulisho na kushushwa kwenye gari la abiria. Wamekamatwa wanaodhaniwa kuwa raia na kufungwa kwenye container, barrier ya Kihomoka Kakonko. Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu. Je kufunga binadamu kwenye container ni halali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi ya Mtende iliishia kumaliza maji Kambini (underground water) kisha wakaja kuomba wachimbe visima vitano kwenye Vijiji vya Kasanda, Kazilamihunda, Kewe, Juhudi na Nkuba. TCRS waliomba kuchimba visima, hivyo waliweka mkataba kuwa wakipata maji lazima wapate host community kwanza (vijiji vitano) kabla hayajapelekwa kambini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maji kupatikana, TCRS walidai hawana bajeti ya kupeleka maji kwenye vijiji vitano kinyume na mkataba. Kijiji cha Kasanda walipata maji toka Water Mission Gate9 na Mkuba Gate2 tu, maji ambayo hayatoshi kabisa na ni kinyume na mkataba. Wananchi wana hasira, chuki na TCRS pamoja na wakimbizi waliochukua maji yao bila wao kupata, jambo ambalo litaleta mgogoro mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wananchi 92 wanaodai fidia ya mazao mpaka sasa hawajalipwa. Suala hili nililifikisha Wizarani ili liweze kufanyiwa kazi, lakini hadi sasa wananchi hao hawajapata fidia yoyote wakati mazao yao yaliharibiwa. Hili linazidi kuongeza chuki kwa wakimbizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uharibifu kwenye barrier ya Kihomoka Kakonko, hutumiwa na Polisi, Uhamiaji na Maliasili. Matumizi yenye uharibifu ni rushwa kwenye magari ya mizigo, abiria wanaodhaniwa kuwa sio raia, rushwa kwa bodaboda, rushwa kwa wafanyabiashara wanaopita barrier hiyo, rushwa kwa wanaobeba mbao, mkaa na kadhalika na kupiga watu bila sababu. Nashauri barrier hii ifungwe, kwani haitendi haki bali kuwafaidisha Polisi na Uhamiaji kwa kujipatia kipato kisicho halali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi Kakonko na nchini kote wanakamata bodaboda wasio na hatia na kuwaomba rushwa kila wakati na kufanya zoezi hili, ni shamba la Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi wengi wa Kakonko wanaomba rushwa kwa raia wanaopatikana na tuhuma mbalimbali na hakuna dhamana bila rushwa. Kituo cha Polisi kina kesi za kubambikiza ili mtu atoe rushwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni Polisi wengi kukaa muda mrefu Kakonko (overstay).