Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami nichangie hoja hii. Kwanza niwapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, IGP, Kamishna General wa Magereza, Kiongozi wa Zimamoto, Kiongozi wa Uhamiaji kwa kazi nzuri wanayoifanya pamoja na Askari wote, wanafanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiona mtu anapambana na Polisi, nashangaa kabisa. Hawa ndio wanaotulinda. Hata hapa Bungeni, saa 24 wanalinda hawa vijana. Nchi yetu hii unatembea saa 24 hata saa 8.00 usiku, usalama upo tu kwa sababu ya hawa Askari. Naomba waongezewe posho zao na wajengewe makazi bora. Sasa hivi makazi wanayokaa kwa kweli yanatisha. Hawa ni binadamu, lazima tuwaheshimu tuwajengee makazi bora kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, Wilaya ya Mpwapwa ina Kata 33, lakini Vituo vya Polisi viko viwili tu pamoja na Makao Makuu ya Polisi Mpwapwa, cha tatu; Kibakwe pamoja na Kipogoro. Kile Kituo cha Kibakwe hawana usafiri. Waliwahi kupewa pikipiki na ile pikipiki imeharibika. Kwa hiyo, naomba IGP tusaidie gari; eneo lile ni kubwa sana, pamoja na Kituo cha Polisi Kipogoro. Wanashughulikia maeneo yote ya Mtera kuhusiana na uvuvi haramu, kwa hiyo, naomba wasaidiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi Mpwapwa Mjini ndiyo Makao Makuu ya Polisi Wilaya. Kituo kile kina zaidi ya miaka 30 hakijafanyiwa ukarabati, paa linavuja. Naomba IGP akitoka hapa atembelee Kituo cha Polisi Mpwapwa. Zile nyumba wanazoishi Askari kwa kweli hazifai, wanaishi tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika mpango wa kujenga nyumba 400 kila mkoa, naomba Wilaya ya Mpwapwa isisahaulike. Tuwajengee Polisi nyumba nzuri hasa hapa Mkoa wa Dodoma. RPC anafanya kazi nzuri, mkoa wake una amani kabisa na utulivu, sisi Wabunge tupo hapa, hatujawahi kutoa malalamiko yoyote kwa RPC, lakini tunaishi vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nawapongeza sana kwa kazi nzuri Askari wote, IGP na vyombo vyote vilivyo chini ya Jeshi la Polisi. Ahsante sana.