Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru pia kuwa mmoja wa wachangiaji wa bajeti hii. Binafsi naunga mkono bajeti ya Kambi Rasmi ya Upinzani iliyozuiliwa kusomwa hapa Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Mpango na Naibu wake kama tulivyosema bajeti hii ni ya kufikirika na sidhani kama itatekelezeka. Kwanza kabisa Deni la Taifa. Wizara hii ndiyo msimamizi mkuu wa Deni la Taifa na mali za nchi. Toka awamu hii imeingia madarakani Deni la Taifa limeongezeka kwa kasi kubwa sana na yeye kama kiongozi anayehusika haoni kama analiletea Taifa hili changamoto inayotusubiri hapo mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwezi ameji-commit na Wizara yake kulipa Deni la Taifa shilingi bilioni 883. Ameji- commit na ana wajibu wa kulipa mishahara ya watumishi karibu shilingi bilioni 617 na kuendelea. Wakati huohuo kuna OC shilingi bilioni 254. Mapato, tukiachia mnavyo-forge maana mmeeleza mapato ni mengi wakati uhalisia si kweli. Matumizi ni 1.7 lakini mapato ni 1.2, hizi nyingine anapata wapi? Kwa hiyo, namsisitiza kwa faida ya Watanzania na hasa wanawake ninaowawakilisha namwomba awe realistic, asiweke figure za kufurahisha viongozi au baraza lake, ahakikishe anaweka figure ambazo zitawasaidia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili, naona niache habari ya Deni la Taifa kwa sababu ni cancer ya Taifa. Nataka niingie kwenye habari ya kilimo. Toka tunapata uhuru tulikuwa tunasema kilimo ni uti wa mgongo na kilimo kinachukua zaidi ya asilimia 65 ya Watanzania, bajeti ya 2016/2017

T A A R I F A . . .

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, mama ni yake wa kambo, kwa hiyo, naelewa anachofanya. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nachotaka kusema ni kwamba 2016/2017 tuliweka bajeti ya shilingi bilioni 1.1 kwa ajili ya bajeti ya kilimo lakini ni shilingi bilioni 3 tu ndiyo zilitoka. Kama unazungumzia kilimo ni uti wa mgongo na sisi kama Bunge tulipitisha hizo pesa tukijua hata kama hazitoshi zinaweza zikasaidia lakini ikatoka shilingi bilioni 3 peke yake. Mwaka huu tunaoumaliza sasa tulitenga shilingi bilioni 150 lakini mpaka leo zimetoka shilingi bilioni 27 peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo ndiyo kila kitu na wewe mwenyewe umetoka kwa wakulima unafahamu, kama pesa haijatoka na sisi Bunge tumepitisha, sioni umuhimu wa kuwepo mahali hapa unless tunafanya siasa. Bunge kama chombo muhimu kimesema pesa kadhaa itoke Wizara haijatoa na wanajinasibu wanakusanya pesa nyingi, sielewi wanasimamia mpango gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kutoa pesa ndogo kwenye kilimo bado kilimo kinaingiza kwenye pato la Taifa takribani asilimia 30 ya pato la Taifa. Kwa nini kama Watanzania tusione umuhimu wa kuwekeza zaidi kwenye kilimo pamoja na viwanda tunavyovizungumzia tukaweza kupata pesa nyingi isiyokuwa na matatizo. Leo hii tuna Vyuo vya Kilimo, kwa mfano, SUA na Uyole huu ni mwaka wa tatu hawajapata pesa za utafiti. Unawezaje kuwa na kilimo safi hufanyi utafiti?

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumza kilimo, tunazungumzia mbegu bora, jana kuna mmoja ametoka kuuliza swali juu ya mbegu za alizeti, mkulima kwa gharama yake anapanda mbegu lakini mbegu haioti. Watafiti hawawezi kusema lolote kwa sababu hawajapewa pesa kwa ajili ya utafiti. Leo hii kuna mbegu za mahindi zinapandwa, hakuna chochote kinafanyika kwa sababu hizo mbegu si mbegu bora lakini hatuwezi kuwalaumu watafiti wetu kwa sababu hawana fedha ya utafiti. Tukienda kwenye mambo hayo hayo ya kilimo, katikati ya kilimo kuna mitamba ile inayotakiwa kufanyiwa utafiti hawajapata pesa. Pale SUA Arusha hawajapata pesa kwa muda mrefu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunazungumzia habari ya kilimo ambacho kimebeba idadi kubwa sana ya Watanzania na mimi ninayewakilisha Mkoa wa Mbeya asilimia kubwa wewe ni shahidi, wanawake ndiyo wanaoingia kwenye kilimo. Kwa gharama zao wenyewe wanaamua kulima, hawana Maafisa Ugani, wako wachache, hawana maelekezo yoyote mwisho wa siku wameshalima lakini masoko pia hamna. Tumeingia kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki wenzetu wamejipanga kwa nini na sisi tusiige, kwa kweli masoko ni shida.

Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi nikisimama hapa nazungumzia suala la chai. Mpaka sasa hatuna viwanda vidogo vidogo vya kusaidia wakulima hawa. Hatuna mkakati wa mbolea au kuwasaidia kwa namna yoyote kama Taifa lakini bajeti inayotengwa ni ndogo na hata hiyo ndogo inayotengwa Wizara haitoi pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii bajeti sijajua walifikiria nini au kuna kitu gani wanakifanya? Hali ya hewa huwezi kuitegemea kwenye kilimo. Tanzania tunaishi kwa kutegemea Mungu anasema nini kwa ajili ya kutuletea mvua. Hatujajipanga kwenye umwagiliaji, hatujajipanga kuhifadhi maji ya mvua, tunasubiri Mungu atoe na asipotoa hatuna kilimo. Naomba sana Mheshimiwa Dkt. Mpango tulitazame suala hili kwa upya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo niende kwenye eneo la wafanyakazi. Sasa hivi imeletwa sheria ya ufutwaji wa Tume ya Mipango. Waziri Mheshimiwa Dkt. Mpango alikuwepo toka awamu iliyopita kwenye Idara hiyo, Marais karibu wanne wamepita hakuna aliyethubutu kufuta hii Idara lakini wanafanya hivyo kwa sababu wanataka wawe huru na kufanya wanavyotaka. Hawataki kuwa na chombo cha kuwasimamia, wanachota hela Bombardier, Chato, hawataki usimamizi. Kwa sababu tukiwa na hii Idara sisi tutaiuliza lakini wanaiondoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Mfuko mmoja wa mapato ya Serikali wanataka ubadilishwe sijajua wanawaza nini. Hatuwezi kumlazimisha maana ameshika mpinina sisi tumeshika makali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, uhakiki wa wafanyakazi umekuwa kwa muda mrefu, kuna sehemu umemalizika lakini kuna watu walipandishwa madaraja miaka miwili iliyopita hawakulipwa mishahara yao. Umefika wakati wa kulipa mishahara yao sawasawa na madaraja waliyopanda
mnawaambia waandike barua kwa wakati mliosema kwa maana miaka ile mingine inapita bila wao kupewa haki yao, huu ni dhuluma na hii ni dhambi mnaipanda kwenye Taifa hili. Jasho la mtu likipotea, kuna wakati hata tunapeleka watoto wetu shule hawafaulu mitihani kumbe ni pesa ya laana. Umempeleka mtoto shule unalipa ada kumbe ile ada uliyolipa kuna watu wanalalamika mahali fulani. Namuonya Mhesimiwa Dkt. Mpango naomba atetee hawa watu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye viwanda, nitazungumzia upande wa Kiwanda cha Ngozi. Hatuna kiwanda cha ngozi na ng’ombe wanagongwa alama tayari hiyo ngozi yao haina thamani. Ng’ombe wanatembea kilometa nyingi, hiyo ngozi haina thamani. Nashauri kuwawekea wafugaji maeneo mazuri ya kulima na kutunza mifugo hiyo ili tupate thamani ya ngozi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda anavyovizungumza Mheshimiwa Mwijage, cherehani tatu anaita ni kiwanda, huku ni kuwachezea Watanzania. Namshauri kaka yangu asifanye vitu kisiasa. Mnapokuwa kwenye cabinet, Mheshimiwa Mwijage nakuamini, shauri hali halisi. Mimi nimegawa vyerehani zaidi ya 400, anataka kuniambia mimi ni mfadhili wa viwanda? Hiyo si sawa. We need the real project, hatuhitaji kufanya vitu kisiasa, kuwanufaisha Watanzania. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la afya ni tatizo hasa kwa magonjwa yasiyoambukiza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.