Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. PAULINE PHILIPO GEKUL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kutoa maoni yangu katika Bajeti ya Serikali iliyokuwa mbele yetu. Naomba nianze mchango wangu kwa kusoma Mwanzo 1:26. Mimi ni Mkristo naomba tu nisome. Inasema: “Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu.”

Mheshimiwa Spika, mzungumzaji aliyepita sasa hivi alikuwa anazungumzia suala la ushirikishwaji, kwamba halmashauri zetu zishirikishwe na Bajeti ya Serikali ishirikishe yote. Hata hivyo, Mheshimiwa Waziri wa Fedha wakati ametuletea Bajeti yake Alhamisi iliyopita, kuna jambo ambalo si zuri sana masikioni mwa Watanzania. Jambo la kumtukuza mtu mmoja kwamba amefanya, amefanya, amefanya, amefanya. Ameanza ukurasa wa tatu (3) akieleza Mheshimiwa Rais kafanya, kafanya mpaka kujenga ukuta wa Mererani kafanya.

Mheshimiwa Spika, Tanzania ni ya kwetu sote na nchi yetu inaongozwa kwa taratibu na sheria. Bunge inapitisha matumizi ya yeyote, mpaka ya Ikulu tunapitisha. Serikali pia inasimamia kile ambacho Bunge tumepitisha na Mahakama pia wanatusaidia. Kwa hiyo, mimi binafsi naona, hayo ni mawazo yangu, kumtukuza sana Mheshimiwa Rais hatumsaidii. Tuongee ukweli kwamba Watanzania wanalipa kodi, kodi hizi zimetumika zimefanya haya na haya na haya na haya. Tuongee tu ukweli, kwamba Bunge limepitisha Bajeti hii; tena Mheshimiwa Spika juzi uliweka vizuri, ukasema kinacholetwa Bungeni ni mapendekezo, Wabunge sisi tuna- amend, tunarekebisha, tunaweka mawazo yetu, tuna-own pamoja kwa sababu Tanzania ni ya kwetu, kuna watu wanalipa kodi, kuna watu lazima wahudumiwe, lakini kusema kwamba Mheshimiwa Rais amefanya, amefanya; mimi…

T A A R I F A . . .

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, naomba niendelee na hapa tunazungumza masuala ya msingi, ni bajeti ya wananchi iko mbele yetu. Kwa hiyo mambo mengine tupunguze tu utani.

Mheshimiwa Spika huu ni ushauri wangu, kwamba ni kweli Rais ameomba kura kwa Watanzania, lakini Rais hafanyi kila kitu. Tusiwe waongo, na tusimtukuze Rais, tumshauri kwa upendo, tumweleze ukweli.

T A A R I F A . . .

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, unajua ukimheshimu mtu muda mrefu sana unaweza ukachoka, ukamvunjia heshima. Huyu mama kuna siku nitachangia Jimbo lake lina matatizo mengi sana. Kuliko majimbo mengine yote, lakini huwa namheshimu sana.

Mheshimiwa Spika naomba niendelee, kwa hiyo naendelea kumheshimu mama yangu. Suala la Rais kafanya, mara elimu bure, mara ukuta, mara hiki. Nchi hii kuna mihimili mitatu, kila mhimili una kazi yake; lakini pia hizi fedha sisi ndio tunaidhinisha. Hata hilo la ukuta wa Mererani ni Kamati zilizopita za Bunge walishauri. Kwa hiyo Mheshimiwa Mwenyekiti, namshauri tu Mheshimiwa Waziri, hatuna sababu ya kumtukuza Mheshimiwa Rais, alishachaguliwa ni vizuri unapoandika…

T A A R I F A . . .

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, ni maamuzi yenu kuendelea kumtukuza lakini hata Mungu katika Mwanzo 1:26 alisema tumfanye mtu kwa mfano wetu. Alihitaji ushirikishwaji, si kutukuza tu mtu mpaka mnapitiliza, ni vizuri mka-moderate, huo ni ushauri wangu.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, Mheshimiwa Waziri tumekuwa tukiongea sana kuhusu Bajeti delivery na disbursement ya fedha zenu kwa Wizara. Bajeti hii ambayo imetekelezwa ambayo sasa wanatueletea leo wametuonesha kuwa kuna baadhi ya Wizara wamewapa fedha kuliko Wizara nyingine zozote.

Mheshimiwa Spika, mfano, Wizara ya Habari, waliwapa bilioni nane kati ya nne; Tume ya Taifa ya Uchaguzi bilioni mbili kati ya sita; Wizara ya Mambo ya Ndani, bilioni kumi na moja kati ya nne; Ofisi ya Makamu wa Rais bilioni tano kati ya mbili; wakati Wizara ya Maji iliomba bilioni mia sita maji ambayo yanagusa maisha ya Watanzania; kila mmoja wetu, bilioni mia mbili mliwapa kati ya mia sita za development.

Mheshimiwa Spika, tumekuwa tukisema kwamba, ni vizuri wakaheshimu maamuzi ya Bunge pale tunapokuwa tumepitisha fedha hizi. Haiwezekani Wizara moja wakaipa zaidi ya asilimia 300 hata Mwaka wa Fedha haujakwisha wakati maeneo mengine hawapeleki fedha. Kwa hiyo ni vizuri, wakaangalia wao wenyewe. Hata Wizara yao juzi wakati wametuletea zaidi ya asilimia 63 wameipa, wametumia sawa, kwa sababu anayekaa na chungu cha ugali ndiye anayekata tonge kubwa, sawa; lakini maeneo mengine hawapeleki fedha na maeneo mengine wanapeleka zaidi ya asilimia 200. Hivi tunawaaminije wa? Kwa hiyo, nahitaji ufafanuzi juu ya hili, kwa nini wanatoa fedha kwa upendeleo.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni suala zima la bajeti hewa, tunapoambiwa hii bajeti ni hewa, ni vizuri tu wakatuelewa. Kwa sababu kazi yetu leo ni kushauri, lakini Watanzania ipo siku wataamua kwamba ninyi mtakaa pembeni na ninyi mtashauri na sisi tutaongoza. Kwa hiyo naomba nizungumze kuhusu bajeti hewa, ni vizuri kwa sababu kila mmoja ana muda wake wa kuchangia. Kila mmoja atashauri, tuna siku saba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, Kamati ya Bajeti ambayo wamekaa nayo muda mrefu sana imeshauri, kwamba mpaka sasa wameweza ku-perform kwa trilioni 20, 10 nzima hawawezi ku-delivery kwa muda uliobaki. Ni kwa nini sasa wanatuletea Bajeti ile ile? Bajeti ya sasa hivi wameongeza bilioni mia tano, on top of bajeti ya mwaka jana. Ni kwa nini sasa wanaongeza bajeti wakati wanajua performance yao ni trilioni 20 kati ya hizo zaidi ya 31, 32, ambazo wanaziomba? Kama wao ni waungwana hawataki tuite kwamba bajeti yao ni hewa hata performance hii ambayo wamekaa na Kamati ya Bajeti japo na Hotuba yetu wameikataa hata haya hawayaoni?

Mheshimiwa Spika, kinachosikitisha, katika fedha ambazo tumezitenga za Development ni trilioni tano tu ndizo wameweza ku-delivery mpaka sasa; hivi wanategemea hii bajeti ambayo wanatuletea kati ya trilioni kumi na moja za maendeleo, tano tu ndizo wamepeleka mwezi mmoja ndio umebaki, hawawezi kufanya, ndiyo maana tunawaambia bajeti hii ni hewa. Ni vizuri wakakubali wakakaa chini wakaiandika upya, tufanye according to kile ambacho tunaweza kukusanya.

Mheshimiwa Spika, TRA wamekusanya mpaka sasa trilioni kumi na mbili, Halmashauri zetu wamekusanya bilioni mia nne kati ya mia sita; lakini wanatuletea wakati wanaona performance ya bajeti hii imefeli. Ndiyo maana tunasema uungwana ni vitendo, wakubali yaishe, kwamba tutumie kile ambacho tunaweza, maana hata mikopo ya wafadhili na zile support tunazopata kwa wahisani zime-drop, fedha haziji. Halafu wanatuletea bajeti ambayo hatuwezi kutekeleza.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya muda naomba tu nizungumzie masuala ya msingi sasa kwenye halmashauri zetu. Mheshimiwa Waziri tulizungumza sana kuhusu halmashauri kuzi-cripple. Wamefanya halmashauri zetu zimeshindwa kufanya kazi; mzungumzaji aliyepita ameongea vizuri. Walivyopitisha bajeti ya mwaka jana kodi ya ardhi, ushuru wa machinjio na hivi vingine wakaona kwamba wafute na vingine Serikali Kuu ikusanye.

Mheshimiwa Spika, kwa hali ya kawaida fedha haziji kwenye halmashauri zetu; OC haziji na kama zinakuja zinakuja kidogo sana. Wakati huo huo hata ile mikopo ambayo halmashauri ilikuwa inapata riba pia wameondoa riba mimi sina tatizo. Kama nia ni njema pia wangekumbuka hata wazee kwenye mikopo ya asilimia 10; lakini kodi ya majengo, kodi ya mabango, mpaka sasa hawasemi kwamba turudishe kwenye halmashauri zetu. Wanachoendelea kufanya wanaendelea ku-cripple halmashauri zetu wanaondoa mpaka na watumishi; halmashauri hizi wameziuwa.

Mheshimiwa Spika, tuliwashauri mwaka jana hawakusikia, mwaka huu wameendelea na business as usual maana yake ni nini? Itafikia hatua nchi hii kila kitu kita-paralyse kwa sababu halmashauri hizi zilianzishwa kwa mujibu wa sheria. Wanatakiwa waziachie halmashauri zetu vyanzo vyao vya mapato.

Mheshimiwa Spika, ni vizuri pia bajeti yetu ika-reflect maisha ya Watanzania. Leo tunavyoongea hii bajeti wanayoleta hapa na vigelegele hapa watumishi hawajawagusa, hakuna increment ya salaries kwa watumishi
... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)