Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, nami nakushuru sana kwa kunipa nafasi niongee kwenye Bunge lako Tukufu, kwa kweli toka tumeanza nilikuwa sijachangia. Leo naomba nianze kwa kuipongeza Serikali, nimpongeze Rais Mheshimiwa Dkt. Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya, nimpongeze Waziri Mpango, nimpongeze Katibu Mkuu wa Fedha, Naibu Waziri, rafiki yangu Ndugu Kichere wa TRA na task force yote kwa kazi kubwa wanayoifanya.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu leo nitaanza na page 47 ambapo Mheshimiwa Waziri ameamua jambo kubwa na la kihistoria kupunguza corporate tax kwa ajili ya viwanda vya ngozi na viwanda vya madawa kutoka asilimia 30 mpaka asilimia 20. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri aende zaidi; kwa viwanda vya ngozi vilivyopo, vinavyokuja, na viwanda vya madawa afanye zero corperate tax. Akifanya zero corporate tax kitakachotokea Tanzania itakuwa hub ya biashara ya madawa. Viwanda vyote vya madawa vitakuja Tanzania kwa sababu itazalisha kwa wingi waende wakauze nchi zote zinazotuzunguka. Viwanda vya ngozi tutaweza kuwa competitives kwenye soko la dunia, lakini tutapata ajira na production itaongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wenzetu huko duniani tunashindana na Mheshimiwa Spika umesema kuhusu Kenya lazima twende kwa kasi zaidi. Kwenye suala la ngozi naomba tuondoe asilimia 10 ya export levy tukiondoa na tu-ban tuhakikishe hakuna kusafirisha tena ngozi ambayo ni raw. Uki- ban raw halafu ukatoa 10 percent na umeondoa corporate tax ni zero, unayo hakika viwanda vyetu vya Tanzania vitazalisha ngozi na vitakwenda kushindana kwenye soko la dunia.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapo kwenye kiwanda nataka niongeze na Kiwanda cha Mbolea. Naombeni Mheshimiwa Waziri tuamue, tuondoe corperate tax iwe zero rated ili watu wote duniani waje wajenge viwanda vya mbolea. Wakijenga viwanda vya mbolea Tanzania kitakachotokea Tanzania ndiyo tuta re- export mbolea kwenye Afrika yote, leo mbolea yote inanunuliwa Morocco, why? Tanzania tuna Gesi, Tanzania tuna Bandari, tunayo sababu tuweke huo mkakati, nina hakika viwanda hivyo vikiwekwa tutapata ajira, production itaongezeka lakini na bei ya mbolea Tanzania itashuka na kwa sababu hiyo tutakipa thamani kilimo.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ambalo leo nitachangia liko page ya 52. Mheshimiwa Waziri ame- introduce electronic stamp, namshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri. Nampongeza na naomba nianze kwa kusema kwenye tax kuna task evasion na tax avoidance. Tax evasion ni kosa la kijinai, tax avoidance ni mtu anatumia sheria zako za kikodi anakwepa kodi na hilo wala siyo kosa la jinai. Tufanye nini ili kuzuia tax avoidance? Mambo mawili lazima yafanyike.

Mheshimiwa Spika, kwanza, kuweka sheria ambazo zitazuia watu wasiweze kukwepa kodi, pili ni kuweka infrastructure ambayo itazuia ama kuweka system watu wasiweze kukwepa kodi. Kwa kufanya hivi tutakuwa tumeenda mbali sana, Waziri wa Fedha ameliona na amelifanya, hongera sana ndugu yangu.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, wako watu watapinga huu mfumo, siyo kwa sababu nyingine yoyote. Mfumo huu unakwenda kufanya yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, mfumo huu unakwenda kufanya production count, kila kitakachozalishwa kwenye kiwanda chochote, TRA wanaona. Jambo la pili kubwa ambalo litatokea kwenye mfumo huu ni revenue itakua. Kila walio-embrace teknolojia hii ya electronic stamp, nchi 47 ninazozifahamu kodi ilipanda kwa asilimia 40 mpaka asilimia 65. Kwa hiyo, naamini mwaka kesho tutakapokutana hapa kodi itakuwa imepanda kwa kiasi kikubwa sana, lakini jambo kubwa ambalo litatusaidia ni bidhaa feki. Kwa wale ambao ni wanywaji kama mimi naomba waniambie ukienda kwenye spirit watu wetu wanakufa sana kwa vinywaji feki. Kwa sababu zile stamp za karatasi kila mtu anaweza akazitengeneza, lakini hapa ni stamp siyo za kutengeneza, kwa hiyo tutaondoa vitu feki na tukiondoa feki wenye viwanda watapata mapato zaidi kwa sababu mapato yao yalikuwa yanashuka kwa sababu ya vitu feki.

Mheshimiwa Spika, wako Watu wanasema tuna hand over sovereignty, sovereignty gani tuna hand over? hapa tunachofanya tunakwenda kuzuia ili Serikali ipate mapato makubwa. Naomba Serikali iendee itekeleze jambo hili na ikiwezekana ipeleke kwenye kila bidhaa, wametuibia inatosha umefika wakati tupate mapato makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hii ndiyo PPP inayosemwa na kuna wenzetu wanaomba PPP lakini PPP zikija naomba hii muitambue hapa amekuja mtu ana fanya self-investment lakini sisi tutapata na yeye atapata, ndiyo maana ya PPP hawezi mtu kuja na technology halafu asipate, haiko dunia ya hivyo. Mtu huyu ameleta hela zake, ameleta techology yake, wewe ghafla unasema na mimi naweza nikafanya mbona hukufanya jana?

Mheshimiwa Spika, ninachoomba sana kwa Serikali jambo hili ni zuri litaongeza ajira. Kubwa zaidi huyu anayekuja kufanya ataajiri Watanzania above all atalipa corporate tax, kwa hiyo revenue itaongezeka both side. Kwa hiyo niombe Mheshimiwa Waziri hili mlisimamie haraka ili liweze kuanza tuweze kupata mapato.(Makofi

Mheshimiwa Spika, jambo lingine nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, toka nimeingia Bungeni mwaka 2005 kila mwaka kwa wale tulikuwepo na Mheshimiwa Spika wewe utasema. Kila mwaka tuliongeza excise duty ya bia, soda, maji pamoja na vinywaji vikali na sigara kila mwaka mpaka tukawa magazeti yanaandika bajeti ya sigara, bajeti ya pombe. Mheshimiwa Waziri wa Fedha ametanzua jambo hilo kwa mara ya kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri na naipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano. Kwa kufanya hivyo maana yake ni nini? Maana yake production itaongezeka, maana yake matumizi yataongezeka, nilikuwa nawatania wenzangu kwa kutoongeza excise duty wale ambao tulikuwa tunakunywa bia mbili sasa tutakunywa tatu kwa sababu zitabakia kwenye bei zile zile tutaweza kutumia hizo bia zetu.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ninalotaka kusema ni kuhusu mafuta ya kula, Waziri wa Fedha amechukua very good measure kupandisha kwenda asilimia 35 na asilimia 25. Sasa nimwombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha lipo jambo la kufanya. Jambo la kwanza lazima aje na extensive master plan ya agriculture ya michikichi pamoja na alizeti. Tusipofanya hivyo bei hizi zitapanda, Wabunge tutarudi hapa kupiga kelele. (Makofi

Mheshimiwa Spika, tumeamua kufunga mkanda, tukitaka kuulegeza mkanda lazima sasa kilimo cha michikichi, kilimo cha alizeti tukipe bajeti. Kwa bahati mbaya sana ukisoma bajeti ya Wizara ya Kilimo hakuna hata senti tano moja inayokwenda kwenye michikichi. Kwa hivyo, inawezekana hii measure ni nzuri lakini ikawa counterproductive.

Mheshimiwa Spika, nami niseme ulikuwa unasema kwa nini Kenya wako mbali? Moja ya sababu ni Kenya wana- embrace commercial farming. Narudia tena mimi siyo muumini wa ujamaa, kama tunataka kilimo kitoke lazima tuanzishe commercial farming. Ukianzisha commercial farming utatoa ajira nyingi zaidi, production itaongezeka kwa sababu yule anayeleta fedha zake atatafuta Wagani wake, atatafuta mbolea na ataongeza production.

Mheshimiwa Spika, ukienda leo michikichi ya Kigoma yote imezeeka, haizalishi mawese tena, ili uweze kuokoa kilimo cha michichiki Kigoma lazima ugawe mbegu mpya. Tukigawa mbegu mpya ndani ya miaka miwili, mitatu tutaweza ku-clear hili gap na mafuta yataongeza.

Mheshimiwa Spika, lingine ni suala la transit trade. ukisoma record za uchumi, sekta mbili zilizoleta fedha Tanzania ni bandari na tourism. Maana yake ni nini? Ili bandari ifanye vizuri zaidi lazima tu-embrace transit trade. Tuondoe vikwazo ili watu wengi watumie bandari ya Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano mafuta yanayokwenda transit trade, mafuta yakiwa yanakuja yakifika Dar es Salaam baada ya siku 30 hayajatoka tunawaambia waya-localise. Ukienda Beira ni siku 90, ukienda Durban siku 120, Walvis Bay siku 90, Mombasa siku 60 maana yake ni nini? Tanzania siyo sehemu ya kwenda kupitisha product hiyo. Tukiongeza siku zikawa 90 maana yake destination ni Dar es Salaam, tutaongeza ajira, tutapata wharfage tutapata storage. Tukipata storage maana yake bandari iende fast, bandari ijenge storage capacity ili tuweze kuweka mafuta hayo. Storage capacity tuliyonayo ilijengwa mwaka 1970, leo ni miaka 47 Taifa limebadilika sana. Ninaomba hilo tulifanye kwa haraka ili tuweze kufanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine nataka kusema PPP project, nimesema kila nilipoingia kwenye Bunge hili, naombeni tubadilishe sheria, naombeni tufanye PPP itatusaidia to easen budget. Hili nalisema kwa sababu nataka leo wenzangu muangalie ukienda page ya 78 ya kitabu cha Waziri wa Fedha ameonesha mfumo wa bajeti ya mwaka wetu. Ukichukua first charge pesa ambazo lazima hata afanyeje Waziri lazima alipe ni trilioni karibu 27 hizi hana choice lazima alipe.

Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye revenue ukatoa mikopo fedha ambazo anaweza akakusanya na hapa maoteo yamepata kwa asilimia 100 ni trilioni 23. Sijaweka OC, sijaweka hela za Development. Unafanyaje katika situation hii? Situation hii lazima uje na PPP, PPP lazima u- embrace concession loan. Kwa mfano, leo Mheshimiwa Rais Magufuli ame-embark kwenye kufanya mambo makubwa mawili ya kihistoria, moja kujenga Reli ya Kimataifa, mbili kujenga Stiglers Gorge jambo kubwa la kihistoria na kwa kweli naamini historia itamuandika Rais Magufuli kwa kufanya miradi hii mikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe ushauri kwa haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, miradi hii tunaijenga kwa fedha za ndani, miradi hii tunaijenga kwa kukopa commercial loans, tukikopa commercial loans maana yake ni moja tu, ukikopa mkopo wa kibiashara unaanza kuulipa ndani ya miezi sita, wakati unaanza kuulipa hata miradi hii haijakwisha, miradi hii haijaleta fedha. Tumeweka seven trilioni mpaka Dodoma lakini mpaka leo tunalipa deni lakini reli haijafika Dodoma. Sasa ili tuweze kupata concession loans lazima tufanye yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, naomba sana, mimi Rais Magufuli namuamini, Rais lazima aende, akutane, afanye mambo ya kidiplomasia. Akutane na Xi Jinping wa China, akutane na Angela Merkel wa German, akutane na Shinzo Abe wa Japan, akutane na Donald Trump wa US, akutane Vladimir Putin wa Urusi, akutane na Theresa May wa UK maana yake nini? Watu wawili wanakutana na mimi najua uwezo wa Rais Magufuli atakwenda na nchi at heart ata-re-negociate for the country tutapata concession loans.

Mheshimiwa Spika, tukipata concession loans maana yake ni moja tu, maana yake tutapata fedha, tutajenga reli yetu, wakati huo hatulipi mpaka baada ya miaka 15 tuwe tunaanza kulipa deni. Maana yake ukienda kwenye figure za bajeti pale kwenye eneo la deni la Taifa la trilioni mbili litapungua, likipungua Waziri wa Fedha atapata fedha sasa ya kupeleka kwenye maendeleo ya vitu vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya yote wenzetu wamefanya, hapa Ethiopia wamejenga reli juzi, tena ni reli inayoenda kwa umeme, wamekopa China concession loan tena one percent. Wakenya wamechukua concession loan, sisi ni nani? Naamini halijaelezwa vizuri, naamini uwezo mkubwa alionao Rais Magufuli hili jambo akiamua litatokea kesho. Tutapata fedha za concession loans, tutafanya miradi mikubwa na maana yake bajeti yetu ya Serikali tutawarahisishia watu wa Wizara ya Fedha ku-balance bajeti.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho ambalo naomba leo nichangie ni suala la Small Business Act. Waziri wa Fedha naomba awape zawadi Watanzania, zawadi hiyo ya kuwapa Watanzania alete Small Business Act. Ni nini maana yake? Tuamue sasa kwenye corporate tax tuweke kitu kinaitwa brackets za kodi kwamba kwa mtu ambaye ana mtaji wa milioni 10 mpaka milioni 100 mtu huyu alipe kodi labda asilimia tano. Kwa mtu ambaye labda ni milioni 100 mpaka bilioni moja alipe asilimia kumi, maana yake ni nini? Tunawa-include watu wote kwenye uchumi. Tukiwa- include watu wote kwenye uchumi tutapata mapato mengi zaidi kuliko yalivyo sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho nikuombe sana nimalizie la mwisho kwangu mimi ni la muhimu sana. Kwenye hoja hii ya viwanda nikuombe kuna measure kubwa wenzetu wa Kenya ambao ni washindani wetu wameweka. Wakenya wameondoa asilimia 30 ya bei ya umeme kwenye manufacturing. Maana yake ni ili viwanda vyao viweze kuwa competitive, tunajenga viwanda, lazima tuweke competition na sisi, tukiondoa hata tuondoe asilimia 40. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie kwa kusema wakati wanajenga kiwanda cha saruji kikubwa Ethiopia, Ethiopia alipewa punguzo la umeme la asilimia 60. Alipopewa punguzo hilo, bei ya saruji ilishuka kwa asilimia 70, here yamefanyika, we are not inventing the wheel. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie kwa kusema nakushukuru sana, naomba niunge mkono hoja, Waziri wa Fedha namuunga mkono, bajeti yetu hii mwaka huu ni nzuri sana ni bajeti inayokwenda kujibu matatizo ya viwanda na matatizo ya kukuza biashara Tanzania.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.