Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru sana asubuhi ya leo na mimi kunipatia nafasi niweze kuchangia mawili, matatu katika bajeti hii ya Tanzania kwa mwaka 2018/2019. Naomba niseme naunga mkono hoja asilimia mia kwa mia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kusema, sasa hivi tuna kaulimbiu ya Tanzania ya Viwanda. Katika kauli mbiu hii naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais anaisimamia kauli yake hii kwa vitendo. Sisi kama Kamati ya Viwanda na Biashara tulipata changamoto mbalimbali za wadau katika maeneo mbalimbali. Katika bajeti ya mwaka huu, naomba nimpongeze sana Waziri wa Fedha changamoto nyingi zimefanyiwa kazi na Serikali, zimefanyiwa kazi na TRA kwa maana hiyo Rais wetu anatekeleza kwa vitendo kauli yake ya Tanzania ya Viwanda. Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na TRA wote nawapongeza sana kwamba sasa tunakwenda vizuri sana katika eneo hili la Tanzania ya Viwanda.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naanza na suala hili la electronic stamp. Naunga mkono hoja, sina matatizo kwani mapato yataongezeka, uhakiki wa uzalishaji utafanyika lakini wasiwasi wangu ni eneo moja la gharama. Kampuni ambayo mnaingia nayo ubia TRA na Serikali kuna viwango wameeleza, kuna dola 6, 10 na 13. Unapozungumzia dola 6 unazungumzia soft drinks, unapozungumzia dola 10 unazungumzia alcohol, unapozungumzia dola 13 unazungumzia spirit, sigara na vitu vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu haina coins ya Sh.10, 20 au 30, tuna coins ya Sh.50 na 100 ambazo nazo ni chache sana. Mimi ni mdau nina Super Market, tuna shida kubwa sana ya coins ya Sh.100 na 200. Leo tunaposema dola 6, huyu bwana atanunua stamp Sh.1,000 atazalisha chupa 1,000, ina maana kila chupa moja imepanda Sh.13. Soda leo inauzwa Sh.500 kwa kutumia utaratibu wa electronic stamp, anatakiwa auze Sh.513, tunapata wapi coins Sh.13? Maana yake ni kwamba wafanyabiashara watauza Sh.550, ile stamp sasa itatoka Sh.13 ya ukweli itakwenda kwenye Sh.50. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye bia wanasema dola 10 sawasawa na Sh.23. Hatuna coins ya Sh.23, atatoka kwenye Sh.23 ataenda kwenye Sh.50 kwa maana stamp sasa pale ni Sh.50. Naomba TRA na Serikali mlifanyie kazi hili, gharama ziko juu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba kidogo niulize swali, je, wakati mna-bargain na hii kampuni, mliwaeleza ukweli wa uzalishaji wa volume za chupa Tanzania? Leo tunazalisha chupa zaidi ya bilioni 10 za soda, juisi, bia na vinywaji mbalimbali, viwanda vimekuwa vingi. Unapofanya biashara na mtu unatakiwa ufanye bargain, volume ya bilioni 10 chupa si volume ndogo. Kama ni dola 6 lazima wapunguze wafanye dola 2 au 3, volume ni kubwa sana ya hizi chupa.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, TRA walikwenda na volume halisi? Walifanya uhakiki kwenye viwanda? Mbona wenye viwanda wanasema hawajafanya uhakiki huo au uhakiki wanatumia uwakilishi wa return zao kwenye TRA? Kama wanatumia uwakilishi wa return za TRA bado liko tatizo. Kwa sababu kuna viwanda vinazalisha lakini hawapeleki return za ukweli TRA, wanadanganya na Kamati tuliwashauri wafanyabiashara wawe wakweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi kwenye upande wa ETS (Electronic Tax Stamp) sina tatizo. Tatizo langu hizo gharama ambazo zipo mwisho zitamwangukia mlaji, Tanzania hatuna coins hesabu zake tutazifanyaje? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa mashine za EFD tumeanza kupata matatizo. Mwezi mmoja nyuma server iliharibika, wafanyabiashara siku nne, tano tulishindwa kupelekea returns reports zetu matokeo yake mapato kidogo yalipungua. Hata leo napozungumza mimi hapa bado ile server haijakaa sawa, EFD bado inasumbua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri wa Fedha amefanya juhudi kubwa, mimi na Mheshimiwa Ndassa tulimwona na tulimpa na ushahidi na tunawasifu sana na Naibu Waziri walifanya kazi kubwa lakini bado server ya EFD haijatengemaa, je, imehujumiwa? Leo Mheshimiwa Waziri ameondoa kodi ya EFD, je, server iko sawasawa? Kama kwenye EFD mashine ndogo hizi tunachemka, je, kwenye electronic stamp tutakuwa na hali gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ushauri wangu tuangalie upande wa gharama. Naunga mkono, itaongeza mapato, itafanya uhakiki, hatutaibiwa lakini tunali-handle vipi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye eneo la pili la industrial sugar. Sisi Kamati yetu ya Viwanda tulipata malalamiko mengi kuhusu refund ya VAT na ile ya 15%. Wafanyabiashara ambao ni Big Five: Cocacola Kwanza Pepsi, Azam, Nyanza Bottlers na Bonite wanaidai Serikali zaidi ya shilingi bilioni 35. Fedha hizi ni mitaji yao ya ndani, hawajapata ile return yao ya 15%. Kamati imewashauri waendelee kuvumilia, Serikali inalifanyia kazi suala lao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu katika eneo hilo, nia ya Serikali ya kudhibiti watu ambao si waaminifu ni njema, ndiyo maana tunawatoza 15% . Sasa tubadilike, badala ya kutoza 15% tuweke penalt, faini ambazo zitasababisha Serikali kupata mapato ya moja kwa moja. Hizi fedha si zetu ni zao, tunatakiwa tufanye refund. Tuweke audit team maalum, kila miezi mitatu iende kwenye viwanda hivi ihakiki Industry sugar imetumika kiasi gani, industry sugar ambayo haikutumika viwandani, wapigwe faini na penalt na ikiwekana wakirudia makosa wafutiwe leseni. Kwa utaratibu huu wa kuchukua refund zao tunawanyima mitaji yao. Leo mitaji mingi imelala Serikalini na wanalalamika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niingie eneo la kilimo (agri- business), nazungumizia kilimo cha biashara. Tanzania tuna eneo kubwa na ardhi nzuri sana, maji ni mengi lakini bado Serikali haijawapanga wananchi na wakulima wake waingie kwenye agri-business. Leo nenda Dubai wana kila aina ya matunda duniani lakini wale supplier wanafanya packaging nzuri, wanaweka matunda yao katika hali ya usafi wanafanya export. Matunda ya Dubai yanatoka Malaysia, Indonesia, India ns Vietnam. Embe linatoka maeneo ambayo maembe ya Tanzania ni mazuri zaidi. Twende kwenye agri- business tuwahamasishe watu wetu ili tusonge mbele zaidi. Katika maeneo ambayo yana ardhi nzuri, rutuba nzuri, mfano Mikoa wa Mbeya na Morogoro, tuna maeneo mazuri ya Mpunga, kwa nini Serikali isihamasishe watu wawekeze kwenye maeneo hayo?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimalizie kwa kusema naunga mkono hoja, yangu mengine yote nitayaandika kwa maandishi. Ahsante sana.