Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Bismillah Rahman Rahiim.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi jioni ya leo, Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango na Naibu Waziri wake na kwa sababu bado tunaendelea na swaumu basi nitazungumza kwa upole na kuwashauri zaidi. Hivi Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri hawa watu wanaposimama wakalalamika kwamba hakuna fedha huko mitaani, Mawaziri wanaposimama kwamba hawajapelekewa fedha, fedha za halmashauri haziendi, fedha zinatumika vibaya hazionekani, hivi wao kama waungwana haya hayawaumi? Kwa nini hawajitathimini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitawashauri leo kwa nini wanakosa fedha, watu wa fedha wataaalam wa mambo ya mahesabu ya pesa wametuambia hapa, kwamba tuna upungufu ya trilioni 1.2 ili kuweza kukidhi mahitaji yetu. Sasa kwa nini hawazipati? Hawazipati kwa sababu wakiwa katika mipango yao bado hawajapanga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme hivi siku zote huwa nazungumza humu, Tanzania kamwe tusitegemee maendeleo kama nchi wakati hatuna National vision, hatuna tunataka nini? Leo wanaizungumzia Tanzania ya viwanda, nikimuuliza Waziri Mheshimiwa Dkt. Mpango katika kipindi cha miaka kumi na Waziri wa Viwanda yuko hapo, katika kipindi cha miaka kumi tunataka viwanda vya aina gani? Vikubwa vingapi? Viwanda vya aina gani, vya kati vingapi? Viwanda vidogo vya aina gani vingapi na mkakati wake upi? Hamna.

T A A R I F A . . .

MHE. YUSSUF S. HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru namheshimu sana msanii huyu. Nazungumza tena atuambie suala la maendeleo ya nchi huwezi kulipima kwa mwaka mmoja au miwili au mitatu. Tukubaliane hapa nawasaidia tukubaliane huwezi kupima maendeleo ya nchi kwa miaka miwili, mitatu, sasa ndani ya mwaka mmoja hadi miaka 10 utuambie tunataka viwanda vidogo hamsini na mkakati wake huu na vitapatikana hivi, hivi, hivi. Tunataka viwanda vya kati ya ishirini vitapatikana hivi na mkakati wake huu. Tunataka viwanda vikubwa vitano vitapatikana hivi, hamna hicho kitu ni usanii tu, sawa. Sasa nawapa really mifano wakajifunze.

T A A R I F A . . .

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Wewe tatizo lako hata kufunga hukufunga. Pilipili usiyoila wewe yakuwashia nini? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaambia hivi, tuwe na huo mkakati. Sasa nawapa mfano mmoja na waende wakajifunze. Huyu Waziri wa mafuta wa Oman alipoingia pale, wale walikuwa wanazalisha mafuta lita 600,000. Alipoingia akakuta wachimbaji wa mafuta yote ni makampuni ya kigeni. Akataka wazawa wachimbe yale mafuta ili ile fedha izunguke ndani ya nchi yao. Akaenda kwa mfalme akamwomba kiasi cha fedha, akawaita matajiri akawaambia kaeni mchimbe mafuta kwa kiwango hiki kinachotakiwa. Asilimia 50 Serikali itawakopesha na asilimia 50 watoe wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi makampuni yanayochimba mafuta Oman ya kizalendo ni 15. Wanazalisha wenyewe, wafanyakazi ni wao wenyewe na kabla ya hapo hawajaanza wao, walitoa vijana wao kwenda kusoma, wakaja wakasimamia, leo wanasimamia uchumi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii kama Serikali wametenga fedha kiasi gani kuwaita wafanyabiashara kwamba wao wanaweza kiwanda kikubwa, waweke kiasi hiki na Serikali itawakopesha kiasi hiki? Tukiwa na viwanda vitatu au vinne kama kile cha Kagera Sugar, kina wafanyakazi zaidi ya 3,000 pale, tukawa na hivyo kumi, tutakwenda wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwa na chini ya vile ambavyo vina wafanyakazi 2,500, tutakwenda wapi? Tukiwa na hivi vidogo tutaenda wapi? Leo unasema wapiga matofali ni kiwanda? Kwa hiyo, ni lazima tufanye hivyo. Tukifanya hivyo, fedha itarudi katika muda mfupi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, huwa nazungumza kwa jazba, achukua mantiki ya ninayozungumza, asichukue ukali wa maneno yangu, huwa nazungumza kwa jazba kwa sababu nazungumza kwa uchungu sana, kwamba kwa nini wenzetu waendelee, sisi tushindwe kuendelea? Kwa hiyo, huo ni mfano mmoja ambao nimetoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano wa pili, hapa wanashindwa kukusanya kodi kwa sababu wameharibu biashara; nchi zote hizi. Mozambique, Malawi, Zambia, Uganda, Rwanda, Burundi na Kenya zilikuwa zinakuja Tanzania kununua bidhaa. Sasa kwa sababu wameharibu biashara, kwa sababu hawajui biashara, wamepandisha kodi, wanataka kukusanya kingi kwa wakati mmoja, badala ya kukusanya kidogo kidogo na Waswahili walisema: ndogo ndogo nyingi, si kubwa moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo toka hapo nje, hao wajasiriamali, hao wadada wanaouza hapo, wanaenda kuchukua bidhaa Uganda. Kwa nini wakati nchi zote hizo zilikuwa zikija Tanzania? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wakija Tanzania kununua maana yake nini? Maana yake hoteli, gesti, migahawa, magari, tunaingiza fedha. Leo wamepandisha kontena hapa hailipiki. Kwa hiyo, bidhaa zile zile zinapita Dar es Salaam, zinaenda Zambia, halafu zinarudi Tanzania zinauzwa. Sisi tunafanya nini? Hivyo ndivyo biashara inavyoendeshwa? Sisi tunazaliwa, hatuna fedha, kwetu siyo matajiri, lakini baba yangu anauza dagaa kwa fungu, anauza malimao, kitunguu na binzari; biashara tunajua. Ndogo ndogo nyingi, si kubwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wao wamepandisha ushuru, wafanyabiashara wameacha kuleta biashara, nchi zote hizi za Maziwa Makuu zilikuwa zinakuja Tanzania kununua biashara, l eo hawaji tena, ni Watanzania wanatoka kwenda kuchukua mashuka na mashati wanakuja kutuuzia Wabunge hapa. Kwa nini? Ni kiasi gani cha fedha tunapoteza? Kwa hiyo, hebu wakae chini wampange, tuone kwa namna gani tunaweza kupata fedha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia suala lingine ambalo litawasaidia kwa haraka kupata fedha. Wameanzisha Reli ya Kati, Bombardier na Stiegler’s Gorge, itawachukua miaka mingapi kurudisha fedha? Nawapa njia nyingine ambayo ni urahisi tu, wataweza kurejesha fedha, ndani ya mwaka mmoja wataanza kuzalisha na kupata fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna ukanda huu wa bahari; Tanga mpaka Mtwara. Wahamasisheni wawekezaji wa ndani, wawawezeshe, waweke miundombinu bora, wahamasishe nje wajenge na Mheshimiwa Naibu Waziri wa Utalii yupo hapa, tujenge hoteli angalau 20 katika ukanda ule. Ndani ya mwaka mmoja, tumejenga hoteli rooms 50, 50 tu, sawa? Baada ya mwaka mmoja, hoteli hizo tayari wageni wanaingia, pesa ile itaanza kurudi. Sasa tunachukua fedha nyingi tunaenda kuikwamisha! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuchukue mfano mwingine hapa, Bunge lililopita hilo wanalosema hao tulikuwa tunazungumzia gesi, gesi, gesi. Ni dola milioni ngapi tumekopa tukawekeza kwenye gesi? Leo gesi tayari tumeiacha, tunaenda kwenye Stiegler’s Gorge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo yake ni nini sasa? Baya zaidi ni pale n ninaposema hatuna vision ni kwamba yale aliyoyaanzisha Mheshimiwa Rais Dkt. Kikwete leo tumeyaacha na ni mamilioni ya pesa, tumeshayaacha tunaanzisha mengine; na haya baada ya miaka 10 akija Rais mwingine yanaaachwa, tunaanzisha mengine. Hili deni la Taifa kila mwaka litaendelea kukua. Wanalaumiwa hivyo, Waheshimiwa hawaoni aibu? Hawaoni tabu kila siku, watu wazima kunyooshewa vidole? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lazima tujipange, tufanye kitu kwa uwezo wetu, tusiongeze kimo kwa kupanda kinu. Hatujafikia huko ambako wanataka kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawapa mfano wa utalii, Dubai tu hapo, wanataka kutoka watalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuchukulie Dubai, wanataka kutoka watalii 5,000,000 hadi watalii 10,000,000; wamewawezesha katika same bank na plan yao wajenge hoteli 150 ikifika 2020. Wana-import kila kitu. Kwa hiyo, baada ya miaka mitano ikifika 2020 ndani ya mwaka 2021 wanaanza kuzalisha. Kwa hiyo, kwa nini hatuigi haya mambo mazuri?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashauri, waangalie mfumo wa biashara, kwa nini wafanyabiashara wetu waende Uganda na nchi zote za Maziwa Makuu wakati walikuwa wanakuja hapa? Leo hawaji, tunapoteza kiasi gani cha fedha? Warudini katika kujenga angalau hoteli 20 au 30 katika ule ukanda, tutazalisha baada ya mwaka mmoja na fedha nyingi tutapata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa kunyooshewa vidole kila siku, watu wazima, sisi wengine inatuuma. Kwa hiyo, nawashauri tuyafanye hayo na tuangalie namna bora. Nami nawaambia tena, katika viwanda hawajajipanga wazee wangu, wajipange vizuri watuambie.