Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SALUM M. REHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia kwenye hotuba hii ya Bajeti Kuu ya Serikali. Kwanza mimi baada ya kuipitia bajeti ningeanza kwanza kujikita kwenye tasnia ya tafiti ndani ya nchi. Baada ya kupitia vitabu na maelekezo ambayo Serikali imesema kimaelezo tu itasaidia na kuhakikisha kwamba inatoa msukumo kwenye tafiti mbalimbali ili kufanya nchi iwe na vitu ambavyo vinaendana na uhalisia.

Mheshimiwa Spika, kitu cha kwanza ambacho ninachokiona kwa kweli kimevunjisha moyo, Serikali haielekezi fedha kwa ajili ya taasisi za utafiti zilizopo nchini, pesa zinatengwa lakini haziendi. Sasa kama fedha haziendi matokeo yake yanakuwa haya; moja, kwenye upande wa kilimo suala zima la uletaji wa mbegu kutoka nchi za nje ndiyo unaotawala. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa inakuwa kama ni mpango maalum wa kuwawezesha makampuni ya nje yakawa yanaleta mbegu nchini kufanya biashara hizo na kuwaacha wazawa hapa ambao wana uwezo wa kuweza kuzalisha hizo mbegu kwa ajili ya mazingira ya nchi yetu wakishindwa kufanya chochote katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeona katika vituo ambavyo vinazalisha mbegu za mahindi tafiti zimeganda zaidi ya miaka miwili sasa hivi wale ambao walitaka kumaliza utafiti wao umekwama, lakini tunaona tatizo kubwa lililopo kwenye suala zima la mbegu za alizeti. Mbegu za alizeti tulizonazo ndani ya nchi hazifai, lazima tuseme ukweli. Ni asilimia 12 tu ya mafuta ambayo yanatoka ndani ya zile mbegu, kwa wenzetu mbegu hizi tunaziita ni makapi.

Mheshimiwa Spika, ukienda nje; leo hii kuna mbegu ambayo ipo Belgium ina uwezo wa kuzalisha mafuta mpaka asilimia 67, kitu ambacho kingeweza kutuongezea mapato lakini kingeweza kutuongezea mafuta mengi ya uzalishaji kama tungeweza kuwekeza katika haya maeneo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niiombe Serikali, katika hayo mazao ambayo ya mkakati ambayo yamekudiwa kuweza kuyawezesha maeneo ya kanda ya kati kuwa ni maeneo ya uzalishaji wa alizeti na kuwa ni sehemu ya mazao ya uchumi, kungekuwa na mtazamo wa aina yake. Kuiwezesha alizeti ya nchini inayozalishwa katika maeneo yetu hapa kutoa mafuta na si kuweza kutoa makapi au mashudu kama ilivyo hivi sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukiweza kuwekeza hapa sasa hivi, tukifanya tafiti za kuzalisha mbegu ambazo zinatoa uwezo mkubwa wa mafuta itaweza kutusaidia kwa kiasi kikubwa sana.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pili, tunahitaji kuzalisha mawese. Mawese tuliyonayo katika nchi hakujawa na mwendelezo wa aina yoyote; Wizara ya Kilimo ipo, watafiti wapo na watu wamesema lakini mbegu zile za mawese za kwetu hizi kutoka Kigoma zimetumiwa kama mother stock kwa nchi mbalimbali duniani ambazo sasa hivi zinaleta mafuta ya mawese katika nchi yetu hii hapa. Kwa hiyo, sisi kama Watanzania tuliotoa zile mother stock tunaletewa mafuta nchini hapa na yanauzwa katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, niwaombe Wizara ya Fedha na Waziri husika, atie msukumo kwenye research ambazo zitaweza kubadilisha tasnia ya uzalishaji wa mbegu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye suala la mbegu za mboga mboga Tanzania imekuwa ni soko kuu la kampuni za Belgium, Uingereza, Switzerland na nchi nyinginezo, hata Kenya, kutuletea mbegu za aina mbalimbali hapa, nyingine zikiwemo za GMO ambazo zinahatarisha na kuongeza kiwango cha kansa kwa mazao ambayo wanakula wananchi wetu hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo wito wangu ni kwamba tuondokane na hii hali, tuweze kuwa na uwezo wa kuzalisha mbegu ambazo zitakubaliana na mazingira yetu na mbolea na udongo tuliokuwa nao na kuwafanya Watanzania waweze kufaidika na kilimo kilichopo nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye utafiti safari hii Tanzania tumeathirika karibu hekta 30,000 kwa American worm au viwavijeshi vya Amerika tunakiita. Hiki kiwavi jeshi kipya kilichokuja hivi karibuni na matokeo yake kuingia tu Tanzania, tumeona athari katika maeneo ya Chemba, Mikoa ya Dodoma, Manyara, Kaskazini kote kwa ujumla, Tanga na maeneo mengine. Sasa wadudu wale au wale viwavijeshi wa aina ile tusifikiri kwamba wamemalizika. Wale sasa hivi mayai wametaga yapo, kama safari hii tulipata athari ya hekari 30,000 mwakani tutarajie zaidi ya hekari laki moja ziaathirika na American worm wale.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wito wangu ninachokiomba tuiwezeshe TFDA na taasisi hizi ambazo zinaweza kushughulika kwanza na udhibiti, upatikanaji wa dawa na mafuta kwa ajili ya kuweza kuwaangamiza hawa wadudu; ziwepo fedha standby ili ikitokea outbreak ya kile kitu tuweze ku-harm kwa nguvu zote kuliko kwamba mnamtafuta Waziri wa Kilimo baada ya athari kuwa imeshatokea, wale wadudu wakiingia siku moja, mbili tatu tayari wameshamaliza maelfu ya heka.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wito wangu ni kwamba tuwezeshe taasisi hizi za utafiti ambazo zinaweza kututengenezea dawa maalum, maana mpaka hivi sasa dawa tunazochukua tunachanganya tu. Hatujawa na dawa maalum kwa ajili ya kuangamiza viwavijeshi vya aina hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, uwezo wa kutengeneza hizo dawa tunao, wapewe wataalam hiyo kazi tuingie maabara ili tutengeneze dawa ambayo itaweza kuwasaidia Watanzania na kuondokana na hili janga. Safari hii athari kubwa imeonekana kwenye mahindi lakini wadudu wale wanakula miche au majani ambayo yana siku kuanzia nne, saba mpaka 25. Vile vile wanakula mpaka ile stem, ule mmea wenyewe wanatoboa ndani katikati pale.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, uwezo wake ni mkubwa tofauti na viwavijeshi wale wa zamani ambao tunaita African worm ambao wale uwezo wao kula hawazidi majani ya siku saba. Kwa hiyo, mazao kama maharage, njegere, kunde na hata mazao mengine madogo madogo ya mtama tujiandae kwamba yanaweza kuangamia kama hatukuchukua tahadhari ya mapema tuka-harm hiyo hali na kuinusuru nchi na kupata janga la njaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wito wangu kwa kweli hizi fedha zilizokuwepo ziwekwe standby kwa kusaidia eneo hili na fedha hizi zilizokuwa allocated ziende, zisiwe nadharia tu za kila siku.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu suala zima la soko la bidhaa zetu. Sisi Tanzania tunazalisha na safari hii projection ya uzalishaji tunaweza kuwa na excess ya mazao zaidi ya tani milioni saba, hayo yamo ndani ya maeneo yetu. Hata hivyo sijaona katika mpango huu kwamba nchi imejipanga vipi kukabiliana nah ii ziada ya mazao ambayo yatakuwa katika maeneo yetu; lengo ni kuwasaidia wakulima wetu. NFRA pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko uwezo wake ni mdogo wa kununua haya mazao na tumeona athari iliyotokea mwaka jana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vile vile ukanda wetu huu wa Afrika Mashariki na nchi nyinginezo za SADC watu wamezalisha, kwa hiyo yale masoko ambayo tulikuwa tumeyatamani kwamba tungeweza kuwapelekea majirani zetu hayapo. Kwa hiyo nchi kama nchi ijiandae sasa kukabiliana na surplus ambayo itatokea katika uzalishaji ambao watu wamezalisha ili tuweze kupeleka mazao yetu nje zaidi na kutanua wigo wa kuwaongezea kipato wakulima wetu hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.