Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii na mimi nichangie hoja iliyokuwa mbele yetu ya bajeti Kuu. Awali ya yote namshukuru Mwenyenzi Mungu aliyetupa afya na uzima, tumefika asubuhi hii ya leo. Nami pia naipongeza Serikali kupitia Wizara hii ya Fedha, Mheshimiwa Waziri, Dkt. Mpango, Naibu wake, Katibu Mkuu na Watendaji wote kwa utendaji wao nzuri na umakini na usimamizi mzuri katika taasisi hii muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo, nami nianze mchango wangu, kama muda utaniruhusu nitachangia mambo matatu. Jambo la kwanza, ni suala la Export Levy, kuvuja kwa mapato na lingine ni hili suala la tax stamp.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza kwa ajili ya Export Levy na ikiwezekana, naweza kutumia muda mwingi sana hapa kutokana na hali ninavyoiona na jambo hili tukiliachia liendelee kama hivi, linaweza kugawa Bunge letu, Serikali yetu, Taifa na upotoshaji ukikaa muda mrefu ambao siyo sahihi. Kuhusu Export Levy ina historia ndefu tofauti na hapa tunavyoanza kujadili. Sababu hizi ziko za kisheria. Kama unavyofahamu, kazi ya Bunge ni kutunga sheria; Serikali kazi yake ni kusimamia sheria na kutekeleza; na Mahakama ni kutafsiri sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumza hapa nina Finance Bill ya Mwaka 2010 ambayo ndiyo tunafanya reference Wabunge wengi, kwamba hizi pesa kama zinaonekana Serikali imeenda kuwapora watu wa Kusini ambao ni pesa zao, walikubali wakatwe kwenye korosho kwa ajili ya maendeleo yao, lakini Serikali hii bila huruma imeenda kuzichukua na kuzipangia matumizi bila kuwashirikisha wenyewe. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, naomba niseme siyo kweli. Kwa mujibu wa Finance Bill ya Mwaka 2010 ambayo ninayo hapa, ilitunga Bunge hili. Naweza kunukuu, Sheria Na. 203 ilianza mwaka 1984 lakini marekebisho yake ya mwaka 2002, 2006 mpaka 2010. 17(a) inasema:

“A person who export raw cashew nut shall pay an export levy to be computed and collected by Tanzania Revenue Authority (TRA) at the rate of fifteen percent of the FOB value.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesitisha. Twende Na. 2 kwenye mgawanyo wake ndiyo kwenye matatizo hapa. Kifungu cha 2 (a) kinasema:

“Sixty five percent would be divided among district council which are cashew nut producer.” Asilimia 65 inakwenda kwenye Wilaya zinazozalisha zao la korosho, lakini bado ni hela ya Serikali. Ukisema inakwenda Wilayani, Halmashauri bado ni Serikali. Siyo hela ambayo unasema kwamba imeporwa kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namba (b), “thirty five percent will be…

T A A R I F A . . .

. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ndugu yangu Mheshimiwa Zitto anavyoniheshimu, nami namheshimu sana, naye anafahamu hivyo, tunaheshimiana sana, nakubali sana maelezo yake, lakini sizungumzi maneno ya mtaani. Nimesema ninayo Finance Bill ya 2010 ndiyo naifanyia reference hapa. Hii hapa na nitai-table mezani ionekane nani anasema ukweli,. si ndiyo! Cap. 203 sawa! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hiyo taarifa yake siipokei kwa sababu mimi naongea mambo ya kisheria. Bahati nzuri, sasa ngoja nieleze kama anavyosema siijui, ni vizuri na Mheshimiwa anajua kabisa kwamba mimi nimeishi kwenye hii. Siongei jambo ambalo silijui siku zote. Nimekaa kwenye korosho miaka 19.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii ilianza mwaka 1984 baada ya zao hili kudorora nchini. Tulifikia uzalishaji wa tani


zaidi ya 174,000, zilishuka mpaka tani 16,000 kwa mwaka. Ndiyo Serikali ya Awamu ya Kwanza ikaamua kuja na mkakati maalum ya kufufua zao hili mwa 1984. Mwaka 1985 ndiyo ikaanzishwa Sheria ya Kuanzisha Bodi ya Korosho (CBT) kwa ajili ya uendelezaji na kufufua zao hili. Mwaka 1990 tulianza kubinafsisha mashirika na kuwa-invite wafanyabiashara binafsi kutoka duniani kote kuja kushirikiana nao kulifufua na kuliendeleza zao la korosho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1994 Kampuni niliyokuwa nafanyia kazi, Olam International ilikuja hapa nchini na ikaanza kununua. Wakati huo Export Levy hii haipo, tulikuwa tuna-export korosho zero rated. Lengo la kufufua hili zao, tuviwezeshe viwanda vyetu 12 alivyojenga Baba wa Taifa mwaka 1978/1979 kwa ajili ya kubangua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikopa mkopo wa World Bank, hivyo viwanda 12 vyote vinajulikana, havikubangua hata korosho. Korosho yote ikawa inaenda nje. Ndiyo likaja wazo la kusema ili tu-discourage kwa ajili ya usafirishaji ya raw nut kwenda nje kufaidisha Mataifa mengine na kuhamishia ajira kule, tuweke Export Levy. Ndiyo ikaja Finance Bill na kubadilisha sheria mwaka 1996. Ndiyo tuliweka ushuru wa kwanza Export Levy three percent. Lengo lilikuwa ni ku- discourage.

T A A R I F A . . .

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani amenipeleka nyumbani. Hili suala la kukusanya pesa zote kwenda kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina haijaanza kwenye korosho. Tulianza EWURA, zote zinaenda Hazina, TCCRA, zote zinaenda Hazina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala waliloleta Finance Bill hapa, kuondoa kipengele namba mbili (2) kwenye matumizi ya pesa zile, nilisema mwanzoni. Kwa mujibu wa Sheria, asilimia 65 ilipaswa iende kwenye Wilaya zinazozalisha korosho zote, zile za Mtwata na Kusini.

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na ukizingatia, unitunzie muda wangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1996 ndiyo ikawekwa 3% kwa ajili ya Export Levy Rate, bado korosho ikawa inaenda more than 90 percent nje. Lengo halijafikia. Ilipofika 2002, Serikali ya Awamu ya Tatu ikaongeza kutoka 3% kwenda 5%, lakini bado korosho ikawa inaenda nje. Ndiyo hapo ulipoanza mgawo. Wakasema kwa sababu lengo kwa kuzuia korosho hizi zisiende nje ni kwa sababu korosho hizi ni chache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri sasa tutungie sheria tuzigawanye, sehemu ya asilimia 65, iende kwenye Wilaya zilizochangia zao hili kufika mapato yao, asilimia 35 ziende CBT wakati huo mfuko ulikuwa haupo kwa ajili ya kuendeleza zao hili ili tunyanyue uzalishaji. Baadaye uzalishaji ukiwa mkubwa, korosho zitaenda nje na viwanda vyetu vitapata. Bado pamoja na na juhudi zote za Serikali hizo, korosho ilikuwa inaenda zaidi ya asilimia 90 nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipofika mwaka 20…

K U H U S U U T A R A T I B U . . .

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa na mchango mwingine mkubwa zaidi zaidi ya huu. Nimekuja kwa sababu lilianza kujadiliwa humu ndani kabla yangu. Sasa tukiacha jambo hilo likae kama lilivyo, umma kule wanaamini walichoongea ni sahihi. Ndiyo maana nimekuja na historia kwanza. Watu wanafikiria tu 2010.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala lilianza 2002, ndiyo mgawo kwa mara ya kwanza ukaanza kuwekwa. Kabla ya hapo ilikuwa inakusanywa. Wakasema asilimia 65 iende kwenye Wilaya, asilimia 35 kwenye CBT kwa ajili ya kuendeleza. Tulipofika 2010, ikaonekana bado korosho zinaondoka nje. Ndiyo ikaja kuongezwa kutoka asilimia 10 iliyoongezwa 2006 kuja asilimia 15 ya sasa. Pamoja na hayo, kwa sababu lengo kubwa ilikuwa ni ku-discourage exportation ya raw, lakini bado korosho zinakwenda wakasema…

Mheshimiwa Mwenyekiti, huo mfuko ambao ulianzishwa kwa ajili ya 2009 na 2010 baada ya sheria kutungwa kwa ajili ya kusimamia addition value na ku-procces hizo korosho hapa nchini, ukafeli na ukawa na matumizi mabovu sana ya pesa.