Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Waziri wa Kilimo. Pongezi pia kwa Naibu Waziri, hakika nawatakia kila lililo la kheri na Mungu awape ziada ya nguvu, hekima, busara na utashi katika kumsaidia Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, shukrani nyingi kwa Serikali kuwakumbuka wakulima wa korosho kwa kuwapunguzia mzigo wa msumari wa kodi/makato mbalimbali katika zao la korosho. Tunaomba Serikali iendelee kuziangalia changamoto zingine zilizopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nia njema ya Serikali kuweka ushuru wa zao la korosho ghafi ziuzwapo nje ya nchi ambayo ilikuwa ni kuendeleza zao la korosho kwa pembejeo, utaalam na kadhalika, imekuwa ikihujumiwa sana. Export Levy inayoratibiwa na Mfuko wa CDTF (WAKFU) inatumiwa vibaya na hovyo. Fedha hizo ni vema zikaenda moja kwa moja kwenye Halmashauri zinazolima korosho ili wajanja wasiturudishe nyuma.