Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kupanga kwa kweli ni kuchagua na uteuzi wa Makao Makuu ya Nchi unaendana na matakwa ya wenye nchi wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba naunga mkono Azimio hili na niwakumbushe tu ndugu zangu historia fupi kwa kifupi tu kwamba mwaka 1891 Mjerumani alipoitwaa nchi yetu kuitawala wakati huo ikiitwa Deutsch- Ostafrika ikiwepo na Rwanda na Burundi, akateua Kijiji cha Bagamoyo kuwa Makao Makuu ya Deutsch-Ostafrika. Wakati huo Bagamoyo ilikuwa na nyumba moja tu ya bati, lakini uteuzi huo ulikuwa na maana ya kuweka changamoto kwamba sasa inajengwa Bagamoyo kuwa sasa ndiyo capital na Jiji la Deutsch-Ostafrika. Baadae ikahamia Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana naomba tu nipongeze uamuzi tu wa kuhamia Dodoma na uamuzi wa kutangaza Dodoma kuwa Jiji, kwamba hii inakamilisha uhuru wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uteuzi wa Dar es Salaam na Dodoma ulikwenda na vigezo vya mkoloni kwamba alihitaji sehemu ambayo atanyonya chochote kilichoko Tanganyika na kukipeleka kwao. Sasa tunajiangalia ndani, tunahitaji Mji Mkuu ambao uko katikati ya Tanzania, ambao utatuhudumia wote kwa pamoja. Ndiyo maana tunaunga mkono uamuzi huu wa kijasiri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimweleze tu kidogo ndugu yangu Mheshimiwa Kubenea anasema kwamba usafiri kuja Dodoma ni mgumu sana. Ni kawaida miji yote ambayo imekuwa mikuu baadae, leo usafiri kwenda Lagos ni rahisi kuliko kwenda Abuja. Safiri kidogo Mheshimiwa Kubenea, usikae tu kwenda Bagamoyo. Vilevile nenda Uganda, usafiri kuingia Entebe ni rahisi kuliko kwenda Kampala. Ni vitu vya kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla muda haujaniishia, nimalizie tu kusema tu, ndugu zangu hebu tumwache Mheshimiwa Rais atekeleze majukumu yake kwa kufuata Katiba hii. Hebu niwasomee tu Ibara ndogo ya 37 ndiyo niishie hapa, inasema; “Mbali na kuzingatia masharti yaliyomo katika Katiba hii na Sheria za Jamhuri ya Muungano katika utendaji wa kazi na shughuli zake, Rais atakuwa huru na hatalazimika kufuata ushauri atakaopewa na mtu yeyote.”