Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nakushukuru kwamba umenipa nafasi ya kuchangia hoja hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Simbachawene tuko Kamati moja ya Katiba na Sheria na anajua jinsi gani Serikali ilivyoshindwa kupeleka fedha za maendeleo katika Wizara nyingine na Ofisi ya Makamu wa Rais iliyolazimishwa kuhamia Dodoma ilivyopewa fedha nyingi sana kinyume/ zaidi ya bajeti iliyoomba. Ni kwa sababu mipango ya kuhamia Dodoma, mipango ya kuufanya uwe Mji Mkuu haikuandaliwa. Tumekurupuka bila kuwa na vigezo, tumekurupuka bila kuwa na takwimu na tunafanya mambo haya kama vile nchi hii inakufa kesho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la kuufanya Dodoma kuwa Mji Mkuu ambayo ndiyo hoja ya Mheshimiwa Simbachawene. Mji Mkuu umetangazwa kabla ya sheria kuja Bungeni. Jiji limetangazwa bila sheria kuja Bungeni. Sasa tunatangaza jiji halafu ndiyo tunaleta sheria, halafu tunapongezana hapa. Tunatangaza Makao Makuu ya nchi Dodoma wakati Jiji la Dodoma halijawa na sheria ya kuifanya Dodoma kuwa Jiji. Maana yake ni kwamba kumbe Mheshimiwa Rais alikuwa anakuja kuhamia kijijini, haji kuhamia kwenye Jiji. Hakuna sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo ni zuri na hakuna anayelipinga, lakini ni lazima tufuate taratibu. Kuna mikoa nchi hii imetimiza vigezo vyote vya kuwa jiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kilimanjaro, Manispaa ya Moshi imetimiza vigezo vyote vya kuwa jiji, lakini Mheshimiwa Rais amekataa Moshi kuwa jiji na Mheshimiwa Simbachawene unajua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine kwa sababu amesema watu wa Kaskazini wasimame kwanza, maendeleo yaende mikoa mingine, yawezekana amekataa Moshi kwa sababu watu wa Kaskazini wasimame kwanza.

T A A R I F A . . .

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni bahati mbaya sana kwamba mtu aliyesimama wala hajui historia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wadau wakubwa wa Moshi ni Baraza la Madiwani, Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kupitia Baraza la Madiwani na Meya wao Japhary Michael ambaye leo ni Mbunge wa Moshi Mjini walipitisha Azimio la Moshi kuwa Jiji. Vikao vya RCC vyote viliamua Moshi iwe Jiji. Anazungumza nini? Nimemsamehe kwa sababu hajui. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maamuzi ya kukurupuka, tunapozungumza hivi leo tunataka Dodoma iwe Jiji, tumeomba msaada wa kujenga uwanja wa mpira kutoka Morocco ili kuifanya Dodoma iwe na hadhi ya Jiji. Madhara yake ni nini? Madhara yake ni kwamba Morocco msimamo wa CCM hawa na Serikali hii kwa miaka yote tokea Baba wa Taifa tunatambua Sahara Magharibi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Dodoma hii watumishi wa umma wameletwa Dodoma. Ndoa zimevunjika, waume wako Dar es Salaam, wake wako Dodoma; wake wako Dar es Salaam, waume wako Dodoma, ndoa zimevunjika. Watu wameshindwa kuhama na wake zao na familia zao, mtu amebakisha miaka minne, leo analazimishwa aje Dodoma kabla ya kustaafu, imekuwa ni shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Dodoma ambayo imetangazwa Mji, Dodoma ambayo imetangazwa Makao Makuu ya nchi haiwezi kuunganisha na nchi za Jumuiya ya Afrika MAshariki. Leo kutoka Rwanda, Waziri akitaka kufanya miadi ya Waziri Mkuu hapa Dodoma akitokea Rwanda hawezi kufika kwa haraka kuliko akifika Dar es Salaam. Hakuna connection kati ya Mkoa wa Dodoma na Mikoa mingine kwa usafiri wa haraka wa anga. (Makofi)

Sasa mnataka Dodoma iwe Mji, Dodoma iwe Makao Makuu, hakuna international schools hapa za kusoma watoto wa Mabalozi. Dodoma haijawa tayari na ninyi mnajua kwamba wapo watu waliofanya research wakasema baada ya miaka 10 ijayo kwa kutenga shilingi trilioni nne kwa kila mwaka kwa muda wa miaka 10…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)