Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niseme kwamba naunga mkono hoja hii ya Mheshimiwa Simbachawene kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangazo la Mheshimiwa Rais siku ile ya sherehe za Muungano kwamba sasa Dodoma limekuwa Jiji, limewafarijisha pia wananchi wa mikoa ya jirani ukiwepo Mkoa wa Singida kwamba Jiji litakapokuwepo Dodoma nao watapata fursa mbalimbali zikiwemo za kibiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutangaza, lakini kabla hajatangaza, alifanya kazi moja kubwa ambayo ilikuwa ni kero iliyopelekea wananchi wa Dodoma kuwa na mtafaruku, mamlaka mbili zilikuwa zinausimamia Mji huu; Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma lakini wakati huo huo kulikuwa na Mamlaka ya CDA. Kwa kuivunja Mamlaka ile ya CDA kumetoa fursa sasa kwa Jiji la Dodoma kusimamiwa na mamlaka moja ambayo itaupanga Mji, lakini kuhakikisha inafanya maendeleo kwa ajili ya wananchi wa Jiji la Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii lakini nikiiomba Serikali ya Jamhuri ya Muungano isaidie Jiji la Dodoma kuhakikisha kama ilivyofanya Jiji la Dar es Salaam, kitengo cha Wizara ya Ardhi kiondoke katika Jiji kiende Wizara ya Ardhi ili kuondoa mtafaruku ambao utakuja kupelelekea squatters tena zianze kuwepo Dodoma. Viwanja vipimwe vya kutosha, miuondombinu ipelekwe, lakini wakati huo huo Halmashauri ya Jiji ishughulikie na ukusanyaji na mapato yake ili kuboresha Jiji ili tuweze kufanya Jiji hili liwe la mfano lakini Jiji la kielelezo kama yalivyo Majiji mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Majiji yetu mengi katika nchi hii yamepangwa vibaya. Jiji hili la Dodoma ikiwa Manispaa, lilikuwa limepangwa vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa naiomba Serikali ije na mchakato katika Bunge hili kuleta sheria ya kutangaza sasa Jiji hili la Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.