Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

MHE. ABDALLAH S. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia kwenye azimio hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wala hatubishani Dodoma kuwa Jiji au siyo Jiji, au Dodoma Kuwa Makao Makuu au siyo Makao Makuu. Tayari hapa ni Makao Makuu na tayari imetangzwa kuwa ni Jiji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji kuwa Jiji is not honorarium privilege, ni vigezo, yaani Mji unakuwa Jiji kwa kuwa na vigezo. Mheshimiwa Simbachawene amekuwa Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI anafahamu Majiji yana sifa gani na Dodoma imepungukiwa sifa gani. Sasa kumuunga mkono Rais kwa hili alilolifanya ya kuifanya Dodoma iwe Jiji kabla haijawa na vigezo vya kuwa Jiji ni kutekeleza vigezo vile kwa vitendo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilitegemea azimio linalokuja hapa liwe la Bunge kuitaka Serikali itenge fedha za kutosha sasa ili twende tukaijenge Dodoma iwe na sifa ya Jiji. Tukisema tu tunapongeza kwamba tayari tumeambiwa na sisi ni Jiji, uneweza ukaitwa Jiji lakini bado ni kijiji. Hii haikusaidii! (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Dodoma ambayo leo ni Jiji haina hata stand ya magari kutoka mkoani; Dodoma ambayo leo ni Jiji haina hata stand ya Daladala, zinasimama kokote tu, zinajipanga humo barabarani. Sasa tunahitaji fedha kuhakikisha Dodoma inapangika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu pekee ya adventure hapa Dodoma ni Mnadani. Mnadani ni kuchafu ajabu! Halmashauri inashindwa hata kutengeza basi. Sawa, tutakuja kuumwa kipindupindu hapa kwa sababu hatuna sehemu nyingine ya kwenda. Weekend lazima uende Mnadani. Unaenda kula, maeneo ni machafu. Halmashauri ibadilishe mindset zake kwamba sasa hivi hapa ni Jiji. Sasa Jiji lina heshima yake na Jiji ni vigezo. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawataka Waheshimiwa Wabunge wa Dodoma watumie fursa waliokuwa nayo kuwa-lobby Waheshimiwa Wabunge hapa tuilazimishe Serikali kutenga fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hazipitiki huko, ikinyesha mvua ni tope kila sehemu. Fedha ya Halmashauri huwezi kujenga barabara zote hizo kwa kiwango cha lami. Barabara ya kilometa moja sasa hivi kwa lami ni kati ya shilingi milioni 900 mpaka shilingi bilioni 1.3. Halmashauri ya Dodoma mna fedha hiyo ya kujenga hizo barabara? Hamna! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyanzo vya maji bado ni kile kile vya Mzakwe, watu wanaongeza, Mji unapanuka, hakiwezi kutosha. Leo mnagawa viwanja, Halmashauri iko busy kutangaza kugawa viwanja. Nendeni mkajenge miundombinu kule watu watakimbilia wenyewe. Unauza viwanja au mnauza mashamba sasa? Kwa sababu ili muuze viwanja na watu wavikimbilie ni lazima mtengeneze barabara, mpeleke umeme, pelekeni miundombinu ya maji, watu watahamia. Leo hata ukijenga kule Mtumba utaenda kukaa? Huwezi kwenda kukaa, tutaendelea kubanana hapa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nafikiri Waheshimiwa Wabunge wa Dodoma mjipange vizuri ili tuweze kuwasaidia tuijenge hii Dodoma. Nasi tunakaa hapa, shughuli zetu tunazifanya hapa, tungependa pawe na hadhi ya Jiji na siyo hii blah blah tunayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.