Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. RUKIA AHMED KASSIM: Mheshimiwa Spika, naanza kwa kusema kuwa Wizara hii ni moyo wa Wizara zote, bila ya Wizara hii Wizara zote haziwezi kufanya kazi. Tunapitisha fedha za maendeleo haziendi kwenye Wizara husika, hakuna Wizara hata moja ambayo fedha za maendeleo zinapelekwa kikamilifu. Kazi na miradi ya maendeleo inashindwa kufanywa, hili ni tatizo kubwa sana. Nashauri Serikali tunapopitisha fedha za maendeleo basi zipelekwe katika Wizara husika.

Mheshimiwa Spika, kushuka kwa thamani ya shilingi yetu kila siku. Shilingi yetu inashuka sana na maisha yanakuwa magumu sana. Biashara hazifanyiki, maduka yanafungwa na hali ya maisha inazidi kuwa ngumu sana. Hivyo basi, naishauri Serikali iangalie nini tatizo lililosababisha mpaka shilingi yetu ikashuka kiasi hiki ili tuweze kurekebisha hii hali isiendelee.

Mheshimiwa Spika, kwenye kitabu ukurasa wa 47 unazungumzia huduma za kibenki na pameandikwa kuwa Watanzania wanaotumia huduma za kibenki wameongezeka na kufikia asilimia 65 mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 57 ya mwaka 2013. Hata hivyo kuongezeka huku kunasababisha baadhi ya wananchi wetu kufilisika, kuna watu wamewekwa chini ya ufilisi. Hili jambo limewatia watu wetu umaskini mkubwa. Serikali iangalie sana hizi benki za kigeni zinazokuja kuwekeza hapa nchini, zinatuletea usumbufu mkubwa sana.

Mheshimiwa Spika, Deni la Taifa kila siku linaongezeka, hili jambo ni kubwa sana, hivyo basi, naishauri Serikali tusiendelee kukopa ni vyema kwanza hili deni likapunguzwa ndiyo baadae tukaendelea kukopa.