Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, suala la ulipaji wakandarasi waliotoa huduma Serikalini limekuwa tatizo kubwa. Wizara imekuwa ikirudia uhakiki hata katika fedha au madai yaliyohakikiwa. Kwa mfano mkandarasi Tanzania Printing Services (TPS) waliotoa huduma ya printing Ofisi ya Waziri Mkuu hadi leo ni zaidi ya miaka miwili kampuni hii haijalipwa kiasi cha shilingi 740,000,000 zilizohakikiwa kati ya shilingi bilioni mbili anazodai.

Mheshimiwa Spika, binafsi nimeongozana na mfanyabiashara huyu Wizarani bila mafanikio, kila mtu anasema file bado lipo internal auditors. Hivi ni lini usumbufu wa kulipa wakandarasi utakoma?

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni usumbufu kwa wafanyabiashara. Leo pale mpakani mwa Tanzania na Zambia imeanzishwa tozo mpya inayoitwa weight and measure ambapo lori moja hutozwa kati ya shilingi 640,000 kwa kupita tu pale.

Mheshimiwa Spika, jambo hili linaongeza gharama za uzalishaji na hivyo kuzifanya bidhaa za Kitanzania kuwa ghali na kushindwa kuhimili ushindani wa soko.