Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango bado haijakidhi kwenye hoja inayohusiana na utekelezaji, inajikita zaidi kupeleka fedha kwenye miradi mipya ambayo haikuwa kwenye mipango ya miaka mitano na badala yake Serikali hii ya Awamu ya Tano inajikita kupeleka fedha kwenye miradi mipya kama ununuzi wa ndege na ujenzi wa ukuta wa Mererani.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa kiwanja cha ndege Chato na ujenzi wa Benki ya CRDB Chato, jengo kubwa la ghorofa Chato. Chato kuna vitega uchumi gani vikubwa vilivyosababisha kupeleka fedha haraka haraka na hii imepelekea malalamiko na baadhi ya miradi kupendelewa kama ya Chato. Usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Mapato ya ndani kupitia Serikali za Mitaa mwaka 2017/2018 yalikuwa bilioni 437.6, asilimia 64 kwa mwaka.

Mheshimiwa Spika, tunaomba ahadi mlizoahidi kupitia Ilani ya CCM mtekeleze kwa wakati na Waziri Mpango uje na majibu ya maswali ya wananchi wanayotuuliza kila siku kwenye mikoa yetu. Kwanza ni lini mtatoa laptop kwa kila mwalimu? Ni lini mtazipeleka shilingi milioni 50 za kila kijiji kwenye vijiji na matumizi na uwazi wa shilingi trilioni 1.5 ziko wapi?