Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, napongeza kwa dhati jitihada za Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wakuu wa Wizara hii kwa kazi ngumu sana waifanyayo kwani mahitaji ni makubwa kuliko pato tulilinalo kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu fedha za maendeleo, naomba kufahamishwa ni namna gani Serikali itafanya au inaona huu upungufu na kuweka mikakati gani ya makusudi ili tuachane na kutegemea mapato ya nje kwa maendeleo yetu. Kwani fedha za maendeleo kwa mwaka 2017/2018 tulikuwa na shilingi bilioni 1,382.98 za ndani na nje shilingi 46,108,149,741 (46.11) na sasa mwaka 2018/2019 ni shilingi bilioni 1,266.03 za ndani na shilingi bilioni 29.18 ni fedha za nje. Ndiyo kusema fedha za nje zikikoma maendeleo yetu nchini yatayumba. Ni vyema Wizara ikaweka mikakati yenye tija zaidi kuongeza mapato ya ndani ya nchi.

Mheshimiwa Spika, lingine ni rasilimali kwa mapato yetu. Naomba tufanye utafiti wa rasilimali za nchi zilizopo kila pande ya nchi yetu kuzibainisha na kuzichimba na kuziongezea thamani hapa nchini kabla ya kuziuza nje.

Mheshimiwa Spika, kwa hotuba ya Mheshimiwa Waziri kuhusu usambazaji wa mafungu ya fedha kuzingatia bajeti iliyopitishwa, hata kwenye mafungu ya Wizara ya Fedha hazikutolewa na baadhi hazikufika asilimia 85. Hii ni dhahiri Wizara nyingine ni dhahama kwa kutekelezewa. Tunaomba Wizara ione namna ya kukusanya mapato ya ndani na kutoa kikamilifu kwenye mafungu ya maendeleo kwa kila Wizara na kwa wakati kama jinsi yalivyopitishwa na Bunge.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa msisitizo wa kuendelea kufanya uhakiki ulio sahihi kwa wakandarasi na wazabuni wetu na kufanyiwa malipo kwa ukamilifu ili tuweze kukamilisha miradi ya maendeleo yetu na ufanikishaji wa huduma ndani ya taasisi zetu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.