Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa dakika zako hapo mezani.

Mheshimiwa Spika, naomba nichangie vitu vichache, katika Halmashauri yetu ya Wilaya ya Kilombero, tuliitwa kikao cha ghafla kuonesha kwamba Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmashauri walikuja Dodoma ili kujumuisha ile miradi ya CGD, kwamba tusiweke kitu kidogo kidogo, tuanzishe miradi mikubwa michache ile hela tuliyopangiwa shilingi bilioni 1.5 ili tutekeleze miradi hiyo kabla ya mwaka wa fedha kwisha.

Mheshimiwa Spika, mpaka leo hiyo pesa haijaisha, kigugumizi kiko wapi? Naomba Mheshimiwa akija hapa Waziri atuambie hiyo hela inapelekwa lini kutekeleza ile miradi michache tuliyokubaliana kama Baraza na wao ndio waliotushauri ili tutekeleze ile miradi waliyoanzisha wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba majibu ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, ndani ya Wilaya ya Kilombero kuna madeni ya walimu yameshahakikiwa na Wilaya ni kubwa, lakini mpaka leo haijulikani hawa walimu watalipwa lini? Sasa watuambie leo katika mwaka huu wa fedha kabla haujaisha haya madeni ya walimu yatakuja kulipwa lini? Wanateseka huko vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndani ya Mkoa wa Morogoro kuna wazabuni ambao wamelisha tender miaka mingi katika taasisi za umma, lakini mpaka leo, hawa watu wanahangaika, wamekopa, wanataka kuuziwa vitu vyao, hela hawajapewa. Wameshafanyiwa uhakiki. Je, ni lini sasa wazabuni wa Mkoa wa Morogoro ambao wanalisha taasisi za umma watalipwa hela zao? Naomba majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, lingine ni wastaafu wa TAZARA. Jimbo langu limepitiwa na wastaafu wa TAZARA na wako wengi kweli ndani ya Wilaya ya Kilombero na huko Mkoa wa Mbeya. Tangu mwaka 2005 waliostaafu mpaka 2009 hawa watu hawajalipwa stahiki zao.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali inasemaje kuhusu hawa wastaafu jamani? Mbona mnawaonea! Wametumikia TAZARA kwa moyo mkuu jamani! Hebu mtoe kauli ya Serikali, ni lini mnaenda kuwalipa hawa wastaafu wa TAZARA? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu kingine hizo shilingi milioni 50 kwenye kila kijiji tunazingoja. Ni lini watatuletea hizo fedha? Wengine tunatoka kwenye vijiji ambavyo hata barabara hamna, magari hayafiki. Labda tungepata hizo, tungepata maendeleo. Ije Wizara hii sasa ituambie ni lini watapeleka hizo hela vijijini? Nadhani hata kwako Kongwa wanazisubiri kwa hamu hizo hela. Je, miaka hii inapita, tutaletewa lini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakusemea na wewe, huwezi kusema hapa, lakini tunahitaji hizo shilingi milioni 50 zifike kwenye kila kijiji ili tuone namna gani wananchi wetu wananufaika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa na hayo tu. Ahsante sana kwa kunipa hiyo nafasi.